TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, May 9, 2013

AZAM KAMBINI KUJIANDAA DHIDI YA MGAMBO
azam d1dcdAzam FC
Baada ya kutolewa katika kombe la shirikisho barani Africa, klabu ya Azam fc maarufu kama “Lambalamba” imesema kuwa sasa imerudisha akili yake katika michuano ya ligi kuu soka Tanzania bara inayoelekea ukingoni kwa msimu huu wa 2012/2013.
Afisa habari wa klabu hiyo, Jafar Idd Maganga amsema kuwa klabu hiyo inaingia kambini katika hosteli zao za Chamazi Mbande, nje kidogo ya jiji la Dar es salaam kujiandaa na mchezo wa jumapili dhidi ya maafande wa jeshi la kujenga taifa kutoka mkoani Pwani Mgambo Shooting.
“Wachezaji wote wamerudi salama baada ya kuhuzunishwa na matokeo ya Morroco, lakini hili ndio soka, tunajua wazi kuwa matokeo yale yaliwashangaza wengi hasa baada ya mchezaji wetu Bocco kukosa penati dakika za lala salama, lakini soka lina mambo yake na sasa tunajiandaa na ligi kuu”. Alisema Jafar.
Jafar alisisitiza kuwa azima yao ni kushiriki kwa mara ya pili michuano ya kimataifa mwakani na ndio maana wanaanza kampeni ya kuchukua nafasi ya pili msimu huu kwa kushinda mechi zilizosalia.
Afisa habari huyo alisema licha ya kutupwa nje na AS FAR Rabat ya Morroco lakini wamejifunza mengi kwani wao bado ni wachanga sana katika mashindano ya kimataifa kwani ndio kwa mara ya kwanza wameshiriki mwaka huu.
Azam fc mpaka sasa wapo nafasi ya pili ya ligi hiyo wakijikusanyia pointi 48 huku nyuma yao wakiwemo simba wenye pointi 42 nafasi ya tatu na leo hii wanashuka dimbani kumenyana na Mgambo Shooting ya Mkoani Tanga katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam. Chanzo: www.fullshangweblog.com

No comments:

Post a Comment