TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, April 22, 2013

WATAALAM WA KILIMO NCHINI WAONGEZEKA WAFIKIA 7,974

Adam-Malima
Na: Benedict Liwenga-Maelezo, Dodoma
Wataalam wa ugani wameongezeka kutoka 3,379 waliokuwepo mwaka 2007 hadi kufikia 7,974 mwezi Juni jana(2012) baada ya Serikali kuajiri wahitimu kutoka vyuo mbalimbali nchini. Hayo yamesemwa leo mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mhe. Adam Kigoma Malima wakati akijibu swali Mhe. Mch. Dk. Getrude Rwakatare (Viti Maalum kupitia Chama cha Mapinduzi).mAmesema kuwa mwaka 2007 Serikali ilifanya tathmini ya
upatikanaji wa huduma za ugani nchini na kubaini kwamba mojawapo ya vikwazo vikubwa vya upatikanaji wa huduma za ugani kwa ufanisi nchini ni upungufu mkubwa wa wataalam.
Malima ameongeza kuwa matokeo ya tathmini hiyo yalionyesha kuwa kulikuwepo na wataalam 3,379 nchini ikilinganishwa na mahitaji halisi ya wataalam 15,082.
Amesema katika kukabiliana na changamoto hiyo , Serikali ilianza kutekeleza Mpango wa kuimarisha huduma za Ugani nchini ambapo kuanzia mwaka 2007 Serikali imevifufua vyuo 13 vya kilimo nchini (MATIs) vilivyo chini ya Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika.
 “Ukarabati mkubwa wa vyuo vitatu MATI Ukiriguru, Maruku na Naliendele-Mtwara na ukarabati mdogo kwa baadhi ya vyuo kumi vingine umefanyika”. Mhe. Malima alisema.
Aidha, Mhe. Malima amesema kuwa vyuo viwili vya mashirika yasiyo ya kiserikali vilishirikishwa katika kutoa mafunzo yaliyolenga kuongeza idadi ya wataalam wa Ugani na vyuo hivo kwa sasa vina uwezo wa kudahili wanafunzi 3,500 kwa wakati mmoja ikilinganishwa na uwezo wa kudahili wanafunzi 600 uliokuwepo kabla ya mwaka 2007.

No comments:

Post a Comment