TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, April 24, 2013

WACHEZAJI SIMBA WAWEKWA KITI MOTO KUHAKIKISHA TIMU INAMALIZA NAFASI YA 3


Benchi la ufundi la Simba jana liliwekwa kitimoto na uongozi wa klabu hiyo kutakiwa kuakikisha  inamaliza ligi katika nafasi ya tatu.

Ofisa habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga alithibitisha kuwepo kwa kikao hicho jana ambapo alisema kilikuwa cha kupanga mikakati ya mechi zilizobaki.  "Ni kweli tulikuwa na kikao jana kati ya benchi la ufundi na uongozi.
"Tageti ni kupanga mikakati jinsi gani tufanye kuakikisha timu yetu inamaliza ligi katika nafasi yatatu. Pia, wao walitoa maoni yao. Kwa hiyo kilichobaki ni utekelezaji kutimiza malengo ambayo tumejiwekea." alisema Kamwaga.
"Azam ambayo inashika nafasi ya pili, wametupita na pointi 11. Kwa hiyo nafasi ya pili itakuwa ngumu kwetu." 

Aliongeza kuwa labda itokee Azam wapoteze michezo yao yote iliyobaki na kisha wao washinde kitu ambacho ni kigumu kwa upande wao.
Simba imebakiza mechi tatu dhidi ya Ruvu Shooting, Polisi Moro, Mgambo JKT na Yanga ambayo akishinda yote atakuwa na pointi 48.
Kwa sasa, Simba inagombea nafasi ya tatu na Kagera Sugar ambayo ina pointi 40 na kubakiwa na mechi mbili. Alisema wamekubali kuwa msimu huu wamepoteza lakini wazishuke zaidi ya nafasi ya tatu hivyo iliwaweze kujipanga kwa ajili ya mwakani

No comments:

Post a Comment