TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, April 23, 2013

UPELELEZI WA KESI YA VITENDO VYA KIGAIDI VYA LWAKATARE WAKAMILIKA


Jeshi la Polisi nchini limekamilisha upepelezi kuhusu kesi inayomkabili Wilfred Lwakatare na mwenzake Ludovick Joseph kuhusu tuhuma za vitendo vya ugaidi vinvyzomkabili. Jalada la kesi hiyo linaandaliwa kupelekwa kwa Mkurugenzi wa Mashitaka nchini, DDP kwa hatua zaidi.

Kaimu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Isaya Mghulu akizungumza na wanahabari leo hii, amesema upelelezi huo umezingatia matukio mbalimbali ya uhalifu yaliyofanyika hapa nchini.
Kuhusu kumwagiwa tindikali kada wa CCM bwana Musa Tesha, katika kampeni za uchaguzi mdogo wa Iguga mwezi Septemba wa mwaka 2011, tayari watuhumiwa wawili wamekwisha kufikishwa mahakamani na upelelezi upo katika hatua za mwisho. Endapo watabainika watuhumiwa wengine, nao watafikishwa mahakamani kwa muda muafaka.

No comments:

Post a Comment