TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, April 26, 2013

LEMA ATIWA MBARONI
lema ee56f
Godbless Lema

Jeshi la polisi mkoani hapa limemtia mbaroni mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godless lema kwa tuhuma za uchochezi kwa wanafunzi  kwenye chuo cha uhasibu mwanzoni mwa wiki katika vurugu zilizotokea chuoni hapo baada ya mwenzao kuuwawa juzi usiku huko maeneo ya njiro jijini hapa.
Akizungumza na vyombo vya habari leo ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani hapa kamishna msaidizi wa polisi Liberatus Sabas alisema kuwa mh.lema alikamatwa huko nyumbani kwake Njiro majira ya saa 9 usiku.
Sabas alisema jeshi hilo linaendelea na mahojiano na mtuhumiwa na kuwa katika tukio hilo zaidi ya watuhumiwa 14 walifikishwa mahakamani jana na kuwa hao hawezi kuwaongelea kwani kesi yao ipo kwenye chombo hicho cha sheria.

Pia kamanda sabas alisema kuwa mh.lema anashikiliwa kutokana na vurugu zilizotokea juzi kwenye chuo cha uhasibu na kuwa atafikishwa mahakamani siku ya jumatatu.
Kwa upande mwengine akijibu baadhi ya maswali ya wanahabari kamanda alisema kuwazaidi ya hao 14 na  Lema hakuna mtuhumiwa mwingine aliyakamatwa kwani ilisemakana wakili wake Albert Msando nae amekamatwa.
Mnamo siku ya jumatatu mwanafunzi mmoja aliuwawa kwenye mitaa ya njiro hali iliyoleta tafrani hadi wanafunzi hao walipoleta vurugu chuo hapa na polisi kutumia mabomo ya machozi kuwatawanya sekeseke hilo lilimalizwa na jeshi la polisi baada ya wanafunzi kutotii amri ya mkuu wa mkoa huo  Magessa Mulongo na kuanza kuingia barabarani kuandamana. Chanzo: www.fullshangweblog.com

No comments:

Post a Comment