TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, April 23, 2013

SAKATA LA JUMA NATURE KUTOLEWA KWENYE INTERVIEW....NATURE AFUNGUKA

Msanii mkongwe na maarufu nchini, Juma Kassin Kiroboto, aka Nature, ameonyesha kukerwa na kile kilichoendelea jana usiku katika kipindi cha burudani cha  televishen inayotizamwa africa ya mashariki alipokuwa akifanya nao interview. Nature alionekana akiwa amevaa kawosh na ndala na mara baada ya mahojiano mafupi ya mwanzo ambapo mtangazaji alisema watarejea baada ya mapumziko mafupi Nature hakuonekana tena. Kilichotokea  kwa mujibu wa Nature mwenyewe, ni wakati wa mapumziko hayo, mtangazaji wa kipindi hicho alimfata na kumuambia kuwa hataendelea na interview tena kwasababu ya mavazi aliyokuwa kavaa ambayo ni ndala na kawosh. kuonyesha kukerwa kwake na ishu hiyo Nature aliamua kuandika kupitia ukurasa wake wa facebook.... 

JUMA NATURE AKAFUNGUKA:
hivi kwa mfano angekuwepo mzungu pale na kavaa
 ndala wangesitisha mahojiano na kuvaa kaoshi ni tatizo,
kunywa nimekunywa bt kuna baya nimeliongea na hivi
 kama kweri we nimuandishi wa habari unaruhusiwa 
kuvaa vile kisheria kama yule mtangazaji nimeboreka 
kinoma na ikiwezekana nasitisha kuanzia ssa
 kupeleka ngoma zangu pale siitaji interview

No comments:

Post a Comment