TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Saturday, April 27, 2013

ARSENAL YASAKA VIFAA
asernal 06070
Arsenal iko tayari kumwaga mpunga kwa ajili ya Stevan Jovetic
 
asernal2 ee0dc
Arsenal pia inamtaka kipa wa Hamburg, Rene Adler

KLABU ya Arsenal imepiga hatua katika mbio zake za kuwania saini ya Stevan Jovetic baada ya kuanza mazungumzo na klabu yake, Fiorentina.
 
Habari zinasema kwamba, kocha Arsene Wenger anaihofia Chelsea kwa namna ilivyopanga kujisuka upya. 

The Gunners wamekuwa wakimfuatilia Jovetic, mwenye umri wa miaka 23, tangu mwaka 2011 na wakati klabu hiyo ya Serie A inamthaminisha kwa kiasi cha Pauni Milioni 25, Arsenal — ambayo ina bajeti ya Pauni Milioni 70 za usajili, inataka ipunguziwe bei ya kumnunua mchezaji huyo.

Hatua ya klabu hiyo kufanya jitihada za mapema kumnasa Jovetic ni dalili nzuri, haswa ikizingatiwa Manchester City na Juventus zote zinamtaka mshambuliaji huyo. Dili lolote litategemea na Arsenal kama itafuzu kucheza Ligi ya Mabingwa msimu ujao.

Wenger, pia anatazamia kumsajili kipa mpya wa kwanza, na amekuwa akimmulika mlinda mlango wa Hamburg, Rene Adler tangu Machi. 

Arsenal inaona kulikoni kutoa Pauni Milioni 15 kuwanunua ama kipa wa Stoke, Asmir Begovic au wa Sunderland, Simon Mignolet, bora kutoa Pauni Milioni 8 kumnasa kipa huyo Mjerumani. 

Wenger anataka kuboresha kikosi chake kujiandaa kupambana na Chelsea ambayo iko mbioni kuwasajili kiungo mshambuliaji wa Bayer Leverkusen, Andre Schurrle na mshambuliaji wa Atletico Madr

No comments:

Post a Comment