TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, October 5, 2012

WALIMU WATANGAZA KUTOADHIMISHA SIKU YA WALIMU DUNIANI

Wakati ulimwengu ukiadhimisha 'siku ya walimu Duniani leo,walimu wa Tanzania hawatakuwa na maadhimisho yoyote kutokana na madai yao ya kutotimizwa pamoja na ahadi ambazo wamekuwa wakiahidiwa na Serikali kila mwaka kwa miaka sita sasa.
Rais wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Gratian Mukoba, alisema tofauti na miaka mengine watahadhimisha siku hiyo wakiwa kazini wakiwa wamekata tamaa ya kuonana na mwajiri wao ambayo ni Serikali kwa kutotimiza madai yao ya msingi.
Alisema madai yao kwa Serikali, ambayo hayajatimizwa hadi sasa ni kuboreshewa mazingira ya kazi, nyongeza ya mshahara inayokidhi hali halisi ya Utumishi wa umma pamoja na kuongezewa posho ya kufundisha.
Aliitaka Sreikali kukubali ushauri wa Bunge na uamuzi wa mahakama ya kazi uliotaka pande mbili kukaa kwenye meza ya majadiliano ili kuendeleza mazungumzo ya namna ya kutatua mgogoro uliopo unaohusu madai ya walimu nchini

No comments:

Post a Comment