TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, October 30, 2012

MKUTANO WA MAJAJI NA MABALOZI WAANZA JIJINI ARUSHA


























Pichani ni Waziri wa sheria na katiba Mathias Chikawe akiwa na Jaji wa mahakama ya Afrika ya haki za binadamu kwenye ufunguzi wa mkutano wa shughuli za mahakama uliowashirikisha mabalozi kutoka nchi za umoja wa Afrika (AU) unaondelea kwenye ukumbi wa hotel ya  Mount Meru jijini hapa(picha na mahmoud ahmad Arusha)

 RAIS wa mahakama ya Afrika( Africa court) kutoka nchini Ghana Sophia Akuffo amefungua mkutano wa kamati ya kudumu ya umoja wa Afrika(AU) uliokutanisha majaji pamoja na mabalozi 54 kutoka nchi za Umoja wa Afrika ulionza leo Akifungua mkutono huo Raisi wa mahakama ya Afrika Sophia Akuffo amezitaka nchi za bara la Afrika kuweka muda na kutekeleza kwa vitendo na kuifahamisha jamii ya waafrika juu ya haki za binadamu na viongozi kuacha kukiuka haki hizo . Alisema kuwa katika mkutano huo washiriki wataweza kuangalia kwa undani mahusiano yaliyopo kati ya mahakama ya kutetea haki za binadamu pamoja na kamati ya wawakilishi ya umoja wa mataifa katika kuhakikisha kuwa mahakama za Afrika zinaboreshwa. Aidha alisema kuwa mkutano huo utaweza pia kuunganisha ushirikiano kati ya mahakama na mashirika mengine ya umoja wa afrika pamoja na kamati ya kudumu ya wawakilishi wa umoja huo ili kuhakikisha kuwa wanafanikiwa katika mambo mbali mbali . “mkutano huu ni muhimu sana kwani majaji na mbalozi wataweza kujadili mambo mazuri ambayo yayawezesha hata mahakama kuondokana na baadhi ya changamoto zinazowakabili”alisema Uwanone Aliongeza kuwa katika mkutano huo wataweza kuweka mkakati juu ya Mahakama na kuweza kubuni njia mbali mbali ambazo zitaweza kulinda haki za binadamu ndani ya afrika. Alieleza kuwa kamati ya wawakilishi ya kudumu ya umoja wa mataifa itaweza kuweka umakini mkubwa kwenye mahakama za Afrka kwa kuwa hiyo ni moja ya sera zilizoko ndani ya umoja wa mataifa. Hata hivyo mkutano huo umehudhuriwa na wadau mbali mbali wa mahakama ya haki za binadamu akiwemo makamu wa rais wa mahakama hiyo ,mwenyekiti wa kamati ya wawakilishi wa umoja wa mataifa pamoja na muwakilishi wa kamati hiyo.

No comments:

Post a Comment