TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, October 2, 2012

SIMU ZA KICHINA ZOTE ZAPIGWA MARUFUKU NCHINI KENYA






















Stori kubwa Kenya ambayo hata kwenye AMPLIFAYA ya CLOUDS FM october 1, 2012 imeshika nafasi ya kwanza ni kuhusu mamlaka ya mawasiliano nchini Kenya kuzizima kiteknolojia simu zote zilizofeki ambazo zimekua zikitumiwa na wakenya.

Mtangazaji wa Citizen Tv/Radio William Tuva ameripoti kwamba wakenya walionunua simu feki wapo kwenye wakati mgumu na itawabidi wanunue simu original kwa sasa ili kurudi tena kwenye mawasiliano.

Ameripoti pia kwamba inasemekana katika mtandao wa simu za mkononi wa Safaricom peke yake ni wateja laki sita ambao wameripotiwa simu zao kuzimwa kwa sababu ni feki.

Kwenye line nyingine Tuva ameripoti pia kwamba Kenya imepoteza mabilioni ya shilingi kutokana na simu feki ambazo zimekua zikiingia sokoni kwa njia ambayo sio halali.

Baadhi ya wananchi ambao simu zao zimefungwa wamekaririwa wakisema waliamka asubuhi na kukuta simu zao hazifanyi kazi, kumbe tayari zimeshazimwa kiteknolojia na tume ya mawasiliano nchini humo ambapo kwa mujibu wa BBC na wateja milioni mbili na nusu ambao simu zao zimezimwa.


Mmoja wa watu hao amekaririwa akisema “usiku ninawekaga alamu nataka saa 11 niamke, sikusikia naamka tu naona nje kunapambazuka na simu yangu wamezima’

No comments:

Post a Comment