SIMU ZA KICHINA ZOTE ZAPIGWA MARUFUKU NCHINI KENYA
Stori
 kubwa Kenya ambayo hata kwenye AMPLIFAYA ya CLOUDS FM october 1, 2012 
imeshika nafasi ya kwanza ni kuhusu mamlaka ya mawasiliano nchini Kenya 
kuzizima kiteknolojia simu zote zilizofeki ambazo zimekua zikitumiwa na 
wakenya.
Mtangazaji
 wa Citizen Tv/Radio William Tuva ameripoti kwamba wakenya walionunua 
simu feki wapo kwenye wakati mgumu na itawabidi wanunue simu original 
kwa sasa ili kurudi tena kwenye mawasiliano.
Ameripoti
 pia kwamba inasemekana katika mtandao wa simu za mkononi wa Safaricom 
peke yake ni wateja laki sita ambao wameripotiwa simu zao kuzimwa kwa 
sababu ni feki.
Kwenye
 line nyingine Tuva ameripoti pia kwamba Kenya imepoteza mabilioni ya 
shilingi kutokana na simu feki ambazo zimekua zikiingia sokoni kwa njia 
ambayo sio halali.
Baadhi
 ya wananchi ambao simu zao zimefungwa wamekaririwa wakisema waliamka 
asubuhi na kukuta simu zao hazifanyi kazi, kumbe tayari zimeshazimwa 
kiteknolojia na tume ya mawasiliano nchini humo ambapo kwa mujibu wa BBC
 na wateja milioni mbili na nusu ambao simu zao zimezimwa.
Mmoja
 wa watu hao amekaririwa akisema “usiku ninawekaga alamu nataka saa 11 
niamke, sikusikia naamka tu naona nje kunapambazuka na simu yangu 
wamezima’

No comments:
Post a Comment