TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, October 24, 2012

MKATABA WA UJENZI WA DARAJA LA KILOMBERO WASAINIWA























 Mtendaji Mkuu wa Tan roads Mhandisi Patrick Mfugale (kushoto) na  Mtendaji Mkuu kutoka kampuni ya ujenzi ya China Railway 15 Bureau group Corporation (CR15G) Zhang Tonggang (kulia) wakiweka saini mkataba wa ujenzi wa daraja la  Kilombero lenye urefu wa  meta 384 na ujenzi wa barabara zake za miingilio za lami( kilometa 9.142)  zoezi hilo litagharimu shilingi bilioni 53.2

Hafla hiyo imefanyika Jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na Waziri wa Ujenzi, Dkt, John Magufuli ,katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Herbert Mrango  Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Tanroads  Bi. Hawa Mmanga , Mbunge wa  Mikumi Abdul Salim Ameir na Mbunge kutoka Morogoro Kusini Innocent Kalgeris .
Ujenzi wa daraja hilo utaziunganisha Wilaya za Mahenge na Ulanga pamoja na kuboresha Usafiri wa mikoa ya kusini  na kuleta kichocheo cha ukuaji wa shughuli za kiuchumi. (Picha na Mwanakombo Jumaa-Maelezo)  
 

No comments:

Post a Comment