TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, October 23, 2012

ALEX FERGUSON NA RIO WAMALIZA MZOZO


















Kocha wa Manchester United Sir Alex Ferguson amesema ameshayamaliza na mchezaji wake Rio Ferdinand ambae weekend iliyopita kwenye game na Stoke City aligoma kuvaa t-shirt ya kampeni ya kupinga ubaguzi wa rangi kwenye soka ambapo ndio alikua mchezaji pekee ambae hakuvaa t shirt ya hiyo kampeni.
Fergie amesema aliaibika kutokana na hicho kitendo cha Rio lakini baadae aligundua ilitokana na tatizo la mawasiliano ila kwa sasa tayari ameshafanya nae mazungumzo hivyo sio ishu kubwa tena manake wameyamaliza ambapo Fergie amesema pia kwamba Rio ataongezewa mkataba wa mwaka mmoja baada ya huu wa sasa kuisha.
Ukiachia Rio Ferdinand ambae mdogo wake Anthony Ferdinand wa QPR alikua na ishu ya ubaguzi kutoka kwa John Terry hivi juzi, zaidi ya wachezaji 30 kwenye Premier League wamepinga hiyo kampeni.

No comments:

Post a Comment