TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, October 26, 2012

MAJINA YA WALIOHUSIKA KUMUUA KAMANDA BARLOW YATAJWA























wandishi wa habari Albert G Sengo kutoka Mwanza ameripoti kwamba majina ya watu watano  wanaotuhumiwa kuhusika moja kwa moja na kifo cha aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Leberatus Barlow yametajwa na Polisi.
Akitaja hayo majina mbele ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Said Mwema, Mkurugenzi wa upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba  amesema simu iliyoporwa ya mwanamama ambaye alikuwa akisindikizwa nyumbani na marehemu ndiyo imesaidia kukamilisha upelelezi huo na wahusika kukamatwa.
Waliotajwa kuhusika na hayo mauaji ni Muganyizi Michael Peter (36) ambaye ametajwa kwamba ndiye aliyemuua Barlow, Chacha Waitare Mwita (50), Magige Mwita Marwa (48),  Buganzi Edward Kusuta pamoja na Bhoke Marwa Mwita (42) ambao wote wamekatwa wakiwa Dar es Saalam walipokimbilia baada ya mauaji.
lisema Kikosi kazi cha upelelezi kilichokuwa chini yake  Manumba kilijigawa kwenye makundi matatu moja ni lile la Ukamataji, Mahojiano na jingine la intelijensia huku wakitumia njia ya sanyansi kufatilia kupitia mitandao ya simu.
 
Kukamatwa kwa watuhumiwa hao wa Dar na wale wa Mwanza kunafanya jumla yao kuwa 10 na bado jeshi linasaka wengine  Lakini chanzo cha hao wauaji kufanya hivyo bado hakijatajwa.
Liberatus Barlow aliuawa Oktoba 13 mwaka huu, saa 8 usiku kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana katika eneo la Minazi mitatu huko Kitangiri wakati alipopita kumsindikiza Mwalimu Dorothy Moses nyumbani kwake kutoka katika kikao cha harusi kilichofanyika Mtaa wa Rufiji.

No comments:

Post a Comment