TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, October 23, 2012

SAKATA LA DAWA FEKI ZA ARV  TAARIFA ZAIDI ZATOLEWA
Waziri wa Afya Dk. Hussein Mwinyi

 Kiwanda cha kutengeneza dawa cha Tanzania Pharmacetical Industrial (TPI) kimesema Serikali inabidi iharakishe uchunguzi kuhusu mtu aliyeingiza nchini dawa bandia ya kupunguza makali ya virusi vya ukimwi iitwayo TT-VR 30 ili kuondoa wasiwasi ulioenea kwa watumiaji.
Mkurugenzi mtendaji wa TPI Ramadhani Madabida amesema uchunguzi wa awali unaonyesha serikali inamfahamu mtu alieingiza hizo dawa Tanzania, zilipotoka na tarehe ya kuingizw hivyo kuharakishwa kwa mchakato huo kutakomesha mizengwe ya baadhi ya wawekezaji kutoka nje kutaka kuchafua ubora wa bidhaa zinazotengenezwa Tanzania.
Tayari serikali imewasimamisha kazi Mkurugenzi mkuu wa bohari ya dawa nchini MSD Joseph Mgaya pamoja na mkuu wa kitengo cha udhibiti ubora na afisa udhibiti ubora wa MSD kutokana na kuidhinisha matumizi ya dawa hiyo bandia ya kupunguza makali ya virusi vya ukimwi.

No comments:

Post a Comment