SAKATA LA DAWA FEKI ZA ARV  TAARIFA ZAIDI ZATOLEWA
![]()  | 
| Waziri wa Afya Dk. Hussein Mwinyi | 
 Kiwanda cha kutengeneza dawa 
cha Tanzania Pharmacetical Industrial (TPI) kimesema Serikali inabidi 
iharakishe uchunguzi kuhusu mtu aliyeingiza nchini dawa bandia ya 
kupunguza makali ya virusi vya ukimwi iitwayo TT-VR 30 ili kuondoa 
wasiwasi ulioenea kwa watumiaji.
Mkurugenzi mtendaji wa TPI 
Ramadhani Madabida amesema uchunguzi wa awali unaonyesha serikali 
inamfahamu mtu alieingiza hizo dawa Tanzania, zilipotoka na tarehe ya 
kuingizw hivyo kuharakishwa kwa mchakato huo kutakomesha mizengwe ya 
baadhi ya wawekezaji kutoka nje kutaka kuchafua ubora wa bidhaa 
zinazotengenezwa Tanzania.
Tayari serikali imewasimamisha 
kazi Mkurugenzi mkuu wa bohari ya dawa nchini MSD Joseph Mgaya pamoja na
 mkuu wa kitengo cha udhibiti ubora na afisa udhibiti ubora wa MSD 
kutokana na kuidhinisha matumizi ya dawa hiyo bandia ya kupunguza makali
 ya virusi vya ukimwi.

No comments:
Post a Comment