TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, October 10, 2012

MAGUFULI ATETA NA MAKANDARASI
WAziri wa Miundo Mbinu John Magufuli azungumza na uongozi wa Kampuni ya Chico
WIZARA ya Ujenzi imewakumbusha Wakandarasi nchini kujenga barabara zinazolingana na thamani ya fedha, iliyopo kwenye mikataba yao.
Agizo hilo limetolewa leo mkoani Singida na Waziri John Magufuli, wakati anakagua marudio ya ujenzi wa barabara, eneo la mlima Sekenke-Shelui, yenye urefu wa kilomita 33.3.
Amesema serikali imetumia zaidi ya Sh.Bilioni 35, kugharamia ujenzi huo, lakini mkandarasi China Henan International Cooparation Group Co Ltd(CHICO), ilijenga chini ya kiwango.
Aidha ameuagiza uongozi wa kampuni hiyo kuwapatia wafanyakazi wake vifaa vya kufanyia kazi, hasa viatu na gloves kwa ajili ya kuvaa mikononi.
Hata hivyo meneja TANROADS Mkoa Singida, Yustak Kangole amesema barabara hiyo baada ya kukamilika Januari, 2008, ilichukua miezi miwili kuanza kubomoka, kutokana na ujenzi hafifu. 
Kwa mujibu wa meneja mradi wa barabara hiyo, mhandisi Stone Chen, marudio ya ujenzi yanaigharimu kampuni zaidi ya S h.Bilioni kumi. 
Na Elisante John 




































No comments:

Post a Comment