TAARIFA KAMILI KUHUSU BOBAN NA NYOSSO KUSIMAMISHWA KUCHEZA SIMBA
Club ya Simba imeleza kuhusu 
kuwasimamisha wachezaji wake wawili ambapo wa kwanza ni Haruna Moshi 
Shaaban (Boban aliesimamishwa kuichezea timu ya wakubwa kutokana na 
vitendo vya utovu wa nidhamu na kutokuwa na heshima kwa mwajiri (timu) 
ambapo klabu imempa muda wa siku 21 kutoa maelezo kuhusu makosa yake 
lakini akishindwa kutoa maelezo ya kuridhisha, klabu inaweza kumchukulia
 hatua zaidi.
Katika kipindi hicho (siku 21 
kuanzia jana), Boban atapokea nusu ya mshahara wake wa kila mwezi na 
hatopata marupurupu yoyote yanayohusiana na timu ya wakubwa
Kwa upande wa Nyoso, uongozi 
umemwagiza afanye mazoezi na kikosi cha timu ya pili (Simba B) hadi 
atakapoimarisha kiwango chake cha uchezaji, hii imetokana na ripoti ya 
benchi la ufundi iliyoonyesha kwamba mchezaji huyo amekuwa akifanya 
makosa mengi ya kiuchezaji yanayoigharimu klabu yake japo amekuwa 
akipewa maelekezo na walimu lakini bado amekuwa akirudia makosa 
yaleyale.
Kutokana na hilo, Nyoso atafanya mazoezi na 
wachezaji wa kikosi cha pili hadi walimu watakaporidhika kwamba 
amejirekebisha na yuko tayari kutumikia kikosi cha wakubwa ambapo kwa 
muda wake wote huo akifanya mazoezi na timu B, Nyoso atakuwa akipata 
mshahara wake wa kila mwezi kama kawaida na pia atapata marupurupu 
wanayopata wachezaji wa Simba B.