TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Sunday, January 20, 2013

WAZIRI MKUU KUHAMASHISHA UCHANGIAJI WA VIKOBA VYA WATU WENYE ULEMAVU
Mh. Waziri Mkuu Mizengo Pinda akimsalimia mtoto Abrahamu Omari (miezi 3) ambaye amebebwa na mama yake mwenye ulemavu wa ngozi anaitwa Amina Fadhilinyuma ya waziri mkuu ni Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Reginali Mengi
ambaye ndiye alianda chakula kwa walemavu katika kukaribisha mwaka mpya 2013.
Mh Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiasalimiana Regina Mengi  mtoto wa Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP .

Mh Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiwahutubia walemavu walio alikwa katiaka cha mchana kilicho anadaliwa na Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Reginali Mengi katika kukaribisha mwaka mpya wa 2013 waziri mkuu alikuwa mgeni rasimi katika  hafla hiyo 

Mh Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiwa anasalimiana na Redds Miss Tanzania Brigiter Alfred amabaye alikuwa ni miongoni mwa wageni walikwa katika kushiriki chakula cha mchana na walemavu kilichoanadaliwa na Mweyekiti wa Makampuni ya IPP Mzee Mengi 























WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema suala la uchangiaji wa VICOBA kwa ajili ya watu wenye ulemavu linahitaji kupangiwa mkakati maalum ili zipatikane fedha za kutosha kuwapa mitaji nao pia wajitegemee.Amesema yuko tayari kukaa na Mkurugenzi Mtendaji wa IPP, Bw. Reginald Mengi ili wabungue bongo ya jinsi ya kutunisha mfuko wa VICOBA kwa ajili ya watu wenye ulemavu.

Ametoa ahadi hiyo leo mchana (Jumapili, Januari 20, 2013) wakati akizungumza na watu wenye ulemavu wa mkoa wa Dar es Salaam katika hafla yao ya chakula cha mchana ya kuukaribisha mwaka mpya 2013 iliyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Hafla hiyo iliandaliwa na Bw. Mengi.

“Bwana Mengi amewasha moto mzuri kwa kuwachangia hawa watu sh. milioni 100. Nimeambiwa kuwa walianza kwa kujichangisha sh. milioni 17. Najua nami nawajibika kuwachangia lakini itabidi nikae naye tuone jinsi huduma hii inavyoweza kusambaa na kuwafikia Watanzania wengi zaidi,” alisema Waziri Mkuu.

Alisema ili uwe mpango endelevu, wabuni mpango utakaowajumuisha Watanzania wengi zaidi, wakiwemo wanasiasa, viongozi wa dini na wengine wengi. “Nia yetu ni kila mwenye nacho achangie ili kuwasadia wenzetu wawe na miradi ya kujikimu kimaisha kupitia mikopo ya VICOBA,” alisema.

No comments:

Post a Comment