TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, January 15, 2013

IFM YAISIFU TANZANIA KWA KUDHIBITI MFUMUKO WA BEI

















Na: Heka Paul- Maelezo

Shirika la Fedha Duniani(IMF) limepomngeza Tanzania kwa usimamizi mzuri wa kisera ambao umesaidia utulivu wa kiuchumi ambao umesaidia kuleta matumaini hatua iliyosababisha mfumuko wa uchumi hapa nchini kuendelea kushuka.
Kauli hiyo Mwakilishi Mkazi nchini wa IMF Thomas Baunsgaard wakati wa mkutano wake yeye na Waziri wa Fedha Dkt. William Mgimwa na waandishi wa habari jijini Dar es salam juu ya kuelezea  tathmini ya mapitio ya mwenendo wa uchumi wa Tanzania iliyofanywa na Shirika la fedha duniani(IMF) .
Alisema kuwa ni muhumu wa kuendelea kudhibiti sera za mapato na matumizi ya serikali na sera za usimamizi wa fedha ili kuwa na uchumi endelevu.
Bw. Baunsgaard alisema kuwa Tanzania imedhamiria kuchukua hatua za ziada ili kuhakikisha inafikiwa lengo la kupunguza mfumuko wa bei hapa nchini.
Aidha alisema kuwa Bodi ya utendaji wa shirika la IMF imeidhinisha nyongeza ya dola za Kimarekani 57 na kuifanya Tanzania kuweza kunufaika na mkopo wenye masharti nafuu toka IMF unaofikia dola zaa kimarekani  114.
Vilevile Bodi iliridhia ombi la Serikali ya Tanzania la kupewa msamaha wa kukuika kigezo cha madeni ya nje yenye masharti ya kibiashara kwa sababu ukiukaji huo hauwezi kuathiri uhimilivu wa deni la Taifa.

No comments:

Post a Comment