TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, January 28, 2013

DROGBA KWENYE MIKONO YA GALATASARAY
Taarifa hii nimeipokea kwamba club ya soka ya Galatasaray imekubali dili la kumsaini mchezaji Didier Drogba kwa miezi la 18 hivyo kumchukua kutoka kwenye club yake ya Shanghai Shenhua.
Mchezaji huyu ambae aliondoka Chelsea last summer imeelezwa kwamba atasaini hilo dili baada ya kumalizika kwa mechi za Ivory coast kwenye AFCON ambapo game yao ijayo inachezwa jumapili ijayo.
Kusaini kwa Drogba na Galatasaray itakua dili kubwa la pili la club hiyo huku la kwanza likiwa ni kumchukua mchezaji Wesley Sneijder kupitia dirisha la usajili wiki iliyopita.

No comments:

Post a Comment