TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, January 15, 2013

TAMKO LA MBATIA KUHUSU KUFANYIWA VURUGU MTWARA

























Mwenyekiti wa  chama cha NCCR Mageuzi James Mbatia amedai kufanyiwa  vururugu katika ziara yake Mtwara na watu wanaodaiwa kutumiwa na baadhi ya wanasiasa.
Mbatia amesema hao watu walianza hizo vurugu kwa kile kinachodaiwa kuwa hawakufurahishwa  na kauli yake ya kuwataka kukubaliana na serikali kutaka gesi ambayo imegunduliwa itoke nje ya Mtwara. 
Mbatia amesema asilimia 90 au 99 ya wananchi walikubaliana na kauli ya kutumia gesi kwa pamoja.
“Tukaelezana vizuri kwamba gesi itakayotoka baharini ambayop ni takribani asilimia 78 ya gesi yote ambayo imeshagundulika mpaka sasa, kituo cha kuisafisha kitakua palepale Mtwara na ikishasafishwa, inasafirishwa na kuuzwa na wanamtwara wanapata mrabaha kwenye hiyo itakayokua inasafirishwa, kimsingi hayo tuliyazungumza na mkutano ulikwenda vizuri, jazba zilishuka na naweza kusema zaidi ya asilimia ya 98 au 99 ya mkutano ule walikua vizuri” – James Mbatia
“Waliofanya fujo ni kikundi cha vijana ambao walikua wameandaliwa na chama cha siasa kwa ajili ya kufanya fujo kwenye mkutano huo, walikua kama 30 mpaka 40 wakawa wanataka maneno maneno lakini sisi tukafanya mkutano wetu vizuri, tukamaliza nikatembea manake ni karibu na ofisi yetu ambapo pia hao vijana walitufata kama kuja kufanya fujo lakini baadae jeshi la polisi likaingilia kati na kuwachukua wachache” – James Mbatia

No comments:

Post a Comment