Umewahi kuona kisiwa kinahama? Hiki hapa, unaweza kuhisi ni Boti au Meli ..!! (+Pichaz)
         
Ubunifu wa binadamu na maendeleo ya 
Teknolojia ni vitu ambavyo huwa vinatuletea mambo mapya kila siku, 
hakuna mtu asiyependa kusifiwa baada ya kufanya kazi nzuri.. ubunifu wa 
hiki kisiwa ni kazi nzuri ambayo tayari pongezi zimeanza kuwafikiwa 
wabunifu walioona kuna umuhimu kuwa na kitu kama hiki cha kuvutia.
Tunajivunia uzuri wa Zanzibar yetu, huo 
ni uzuri kwenye kisiwa cha asili kabisa.. taarifa ikufikie kwamba wapo 
waliowaza kutengeneza kisiwa kinachohama kwa kutembea juu ya maji kama 
ilivyo meli au Boti.
Najua kwamba Dunia inavitambua pia visiwa vilivyotengenezwa na binadamu ikiwepo Palm Island, ambacho kiko Dubai… lakini Dunia inatambulishwa pia kwenye Kisiwa ambacho kimebuniwa na wataalam wa Kampuni ya Migaloo ambao wanadili sana na kutengeneza Boti za kifahari.
Ubunifu huu utasogezwa kwenye Maonesho maalum ya Monaco Yatch Show
 na tayari watu wenye pesa zao wameonekana kuvutiwa sana na hii kitu, 
kwa hiyo tayari ni biashara ambayo inatarajia wateja wa nguvu kabisa any
 time kuanzia sasahivi !!

Ukiangalia nje mpaka ndani Kisiwa hiki 
kinavutia, na kina mahitaji yote muhimu kwa mtu anayehitaji kuishi ndani
 yake, kwenye vilivyomo unaambiwa mpaka Beach za nguvu kabisa zipo ndani
 !!


Hii
 ni Beach ambayo iko kwenye kisiwa hicho cha kisasa kabisa, na ardhi 
ambayo iko kwenye kisiwa ni kama ambayp iko kwenye maeneo yenye hali ya 
kitropiki.


Juu kwa juu mtu wangu, hapo kuna Beach ya nguvu kisiwani, Bustani na miti.. vyote vinaongeza uzuri wa Kisiwa hiki.

Ndani
 kunavutia mtu wangu, yani huku ndani unaambiwa kuna Beach nyingine na 
mazingira poa kabisa ya kujienjoy !! Ukiingia mpaka unajisahau kwamba 
uko kwenye kisiwa kinachoelea.
Ubunifu huo wa nguvu huu hapa pia kwenye video mtu wa nguvu, teknolojia ina mazuri yake ya kuvutia kila siku yani !!


No comments:
Post a Comment