TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, September 9, 2015

Baada ya kufikia rekodi ya Sir Bobby Charlton, Wayne Rooney kwenye headlines na rekodi hii

Mshambuliaji wa klabu ya Manchester United na timu ya taifa ya Uingereza Wayne Rooney, siku kadhaa nyuma alifikia rekodi ya mfungaji bora wa muda wote wa timu ya taifa ya Uingereza Sir Bobby Charlton, usiku wa September 8 alivunja rekodi ya Sir Bobby Charlton kwa kufunga goli la 50.
2C1693CD00000578-3226944-image-a-70_1441746439612
Wayne Rooney alifunga goli la 50 kwa mkwaju wa penati  akiwa na timu yake ya taifa ya Uingereza wakati wa mchezo dhidi ya Switzerland wa kuwania kufuzu kucheza EURO 2016, mechi ilimalizika kwa Uingereza kuibuka na ushindi wa jumla wa goli 2-0.
2C16903E00000578-3226944-image-a-71_1441746470439
Baada ya mechi hiyo Rooney aliingia katika chumba cha kubadilishia nguo huku akipigiwa makofi na wachezaji wenzake pamoja na kocha na kukabidhiwa jezi namba 50 ambayo ni jumla ya magoli aliyofunga katika timu ya taifa ya Uingereza.
2C16911600000578-3226944-image-a-77_1441746577925
22

No comments:

Post a Comment