TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, September 15, 2015

Hii ni rekodi inayoipeleka Juventus kinyonge katika mechi yake dhidi ya Man City…(+Pichaz)

Klabu ya Juventus ya Italia tayari imewasili jijini Manchester kwa ajili ya mchezo wake wa kwanza wa hatua ya makundi dhidi ya klabu ya Manchester City katika mechi yake ya kwanza ya Kundi D. Licha ya kufika fainali ya Ligi ya Mabingwa msimu uliyomalizika, klabu ya Juventus haijaanza vizuri katika mechi zake 3 za Ligi Kuu Italia.
2C5046B800000578-3233875-image-a-16_1442254319564
Juventus wamecheza mechi tatu hadi sasa za Serie A, mechi dhidi ya Udinese na kupoteza kwa 1-0 wakiwa nyumbani, baadae kufutia kwa kipigo cha pili cha goli 2-0 kutoka kwa Roma kabla ya mechi yake ya tatu kucheza na klabu ya Chievo na kuambulia point moja baada ya kutoka sare ya goli 1-1.
2C5042BE00000578-3233875-image-a-17_1442254363939
Licha ya kuwa na mwanzo mbaya wa Ligi Kuu ukilinganisha na wapinzani wao Man City ambao wanaonekana kuwa vizuri kwa kufanya vizuri katika mechi zao 5 za Ligi Kuu Uingereza na kuongoza Ligi hiyo, kocha wa Juventus Massimiliano Allegri tumaini pekee linalombeba na kuipa presha Man City ni rekodi yake ya kufanya vizuri msimu uliyopita katika Ligi ya Mabingwa.
2C505F5800000578-3233875-image-a-18_1442254443561
2C503E6D00000578-3233875-image-m-20_1442255004444
2C4D28A000000578-0-image-a-52_1442231237712

No comments:

Post a Comment