TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, September 3, 2015

Jorge Mendes ndiye jamaa anayevuna pesa nyingi katika kipindi cha usajili

Ikiwa ni siku moja toka dirisha la usajili lifungwe barani Ulaya, kila klabu inajiandaa kupiga mahesabu ni kiasi gani cha fedha imetumia kwa ajili ya kufanya usajili. Lakini wakati vilabu vikipiga hesabu ya kiasi gani imetoa na kuingiza wakati wa usajili, kuna mtu anaitwa Jorge Mendes yeye wakati huu, huwa anapiga hesabu ya kiasi alichoingiza.
jorge-mendes_3023686b
Jorge akiwa na Radamel Falcao ni wakala wake pia
Jorge Mendes ni wakala maarufu ambaye anafanya shughuli hiyo kwa wachezaji kadhaa, huwa anatanguliza maslahi mbele kuliko kitu kingine chochote. Kati ya mwaka 2001 hadi 2010 amehusika kwa asilimia 68 katika kila usajili wa kuuza wachezaji kutoka vilabu vya Benfica,Porto na Sporting Lisbon za Ureno.
1356645085_extras_mosaico_noticia_1_g_0
Ni wakala wa Pepe pia
Mreno huyu kwa hivi siku za karibuni amekuwa ana husika kwa nafasi kubwa katika usajili unaofanywa na vilabu vya Atletico MadridDeportivo La CorunaMonaco na Valencia. Huyu ndiye wakala ambaye mara nyingi ufaidika katika uhamisho wa masaa kadhaa kabla ya dirisha la usajili kufungwa.
1356645085_extras_mosaico_noticia_1_g_0
Haikuwa safari rahisi kwa Jorge Mendes kuwa wakala mkubwa wa wachezaji wa kubwa, safari ilianza mwaka 1996 kwa mteja wake wa kwanza Nuno walipo kutana katika Bar ya Guimaraes na kufanikisha uhamisho wa Nuno kwenda katika klabu ya Deportivo . Mendes ni wakala wa Cristiano Ronaldo na wachezaji wengine wengi.
Diego Costa ni moja kati ya wateja wa Mendes hiki ni kitu alichowahi kufanyiwa na Mendes katika masuala ya usajili.
Manchester-City-vs-Chelsea
“Jorge aliniambia natakiwa kupanda ndege na kwenda Madrid lakini nilikuwa sijui nini kinaendelea nilivyofika aliniambia alikuwa anasaini Atletico Madrid, baadae akaniambia kuwa tulikuwa katika nyumba ya mkurugenzi wa michezo wa Atletico Madrid  Jesús García Pitcarch nilikuwa simjui hata kidogo”>>> Diego Costa
*** Local Caption *** BEBE-AGENT: Jorge Mendes er agenten til blant annet Manchester Uniteds Nani.
Ameshawahi kusimamia uhamisho wa Luis Nani
Kama utakuwa unakumbuka vizuri Jorge Mendes ndiye wakala aliyepewa zawadi ya kisiwa  na Cristiano Ronaldo katika harusi yake, kupitia biashara hiyo katika kipindi cha miaka 20, Mendes anatajwa kuingiza kiasi cha pound bilion 1 na anatajwa kama wakala ambaye mipango yake ya uhamisho mingi huwa inafanikiwa

No comments:

Post a Comment