TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, September 2, 2015

Dau la usajili wa Anthony Martial Man United lamfanya Wayne Rooney aulize maswali haya…

Klabu ya Manchester United ya Uingereza ipo karibuni kumsajili mshambuliaji chipukizi kutokea Monaco ya Ufaransa, licha ya kuwa bado haijathibitika kuwa wamemsajili ila tayari Anthony Martial ameripotiwa kufanya vipimo vya afya katika klabu ya Manchester United.
453081752-e1407478205505
Anthony Martial anaripotiwa kusajiliwa na Man United kwa dau la pound milioni 36, kulingana na umri wake kuwa mdogo, kiasi hicho kinatajwa kuwa sio cha kawaida kiasi kwamba kimepelekea nahodha wa timu hiyo Wayne Rooney kushituka kidogo na kumuuliza Morgan Schneiderlin kuhusiana na mshambuliaji huyo.
Martial-nvo
“Kiukweli wakati tupo katika ndege Wayne Rooney alikuja kuniuliza Martial ni nani? kwa sababu magazeti ya Uingereza yalikuwa yakimzungumzia, nilimwambia ni mchezaji mzuri ana uwezo mkubwa  na alicheza mechi kadhaa na Monaco msimu uliyopita na mwanzoni mwa msimu huu”>>>Morgan Schneiderlin
“Nilimwambia Rooney kiufundi yupo vizuri na anafananishwa na Thierry Henry hata hivyo ni kwa mujibu wa magazeti ndio yanayomfananisha na Henry”>>> Morgan Schneiderlin
Anthony-Martial-Monaco
Anthony Martial ni mchezaji mwenye umri wa miaka 19 hivyo wengi ulinganisha kiasi cha fedha na umri wake, kwani mara nyingi mchezaji anaye nunuliwa kwa dau kama hilo ni mchezaji mkubwa au kama mdogo ni lazima awe na uwezo mkubwa, hivyo ndio maana Rooney amebidi aulize kuhusiana na mchezaji huyo.

No comments:

Post a Comment