TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, April 13, 2015

Watanzania waingia, waishi China kinyemela

Balozi wa Tanzania nchini China, Abdulrahman Shimbo
Balozi wa Tanzania nchini China, Abdulrahman Shimbo.
WATANZANIA wengi wametajwa kuingia na kuishi nchini China kinyemela na kusababisha wanapopata matatizo yanayohitaji msaada wa serikali kushindikana kupewa, kwa kuwa hawamo katika utaratibu wa Diaspora.
Balozi wa Tanzania nchini China, Abdulrahman Shimbo alisema lipo tatizo kubwa kutokana na Watanzania wengi kuingia kinyemela kuishi, wakifanya biashara zisizo na vibali na wengi wao ni mama lishe na wafanyabiashara ndogo.
Aidha, amehadharisha juu ya Watanzania kujikuta wakisoma kwenye vyuo visivyo na ubora nchini hapa kwa kutaka wanaosoma vyuo vikuu mbalimbali wasaidie kutoa taarifa muhimu.
Shimbo alisema hayo jana alipozungumza na viongozi wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Tanzania Beijing (TZ-SUB) katika kikao cha makabidhiano ya uongozi mpya na utoaji vyeti kwa Tume ya Uchaguzi ya Jumuiya hiyo.
Kikao hicho kilifanyika ubalozini na uchaguzi ulifanyika Aprili 5, mwaka huu ubalozini pia.
Akizungumzia Watanzania wanaoingia kinyemela China, Shimbo alisema, “Wanaishi hapa, hawakamatwi ingawa hawana nyaraka muhimu, kwa kuwa wengi wao wanasaidiwa na Wachina wenyewe wasio waadilifu. “Wengi ni mama lishe, wakipata shida sasa wanaanza kuitafuta serikali, unaanzia wapi kumsaidia mtu wa aina hii, ni shida na suala la vibali kwa wenzetu hapa wapo makini kweli kweli.”
Alitaja miji yenye tatizo hilo kwa kiwango kikubwa ni Guangzhou na Hong Kong. Aliwataka Watanzania kujiandikisha ubalozini wanapofika nchini hapa na pia kuhakikisha wana vibali muhimu vya kuwawezesha kuishi ugenini.
Kuhusu masuala ya elimu, Balozi aliwataka wanafunzi Watanzania wanaosoma katika vyuo vikuu mbalimbali nchini hapa, kusaidia taasisi za elimu na wizara kutoa taarifa muhimu kuhusu vyuo nchini hapa kusaidia kupunguza wimbi la watu wanaotumia vibaya nafasi hiyo kuwapotosha watu na kujikuta wanasoma katika vyuo visivyo na ubora.
“Wasaidieni nyumbani kujua vyuo bora, kuna watu wanakuja hapa wanasoma miaka minne lugha, hawana hati wala maendeleo yao hayajulikani. “Wengine wanaishi maisha yasiyoeleweka, hujui kama ni wanafunzi ama la, hii ni hatari kwao na mustakabali wa elimu kwa taifa letu, nyie mmekuwa hapa mnaijua nchi hii vizuri, wasaidieni tafadhali,” alisisitiza Balozi Shimbo. CHANZO: BBC (Muro)

No comments:

Post a Comment