TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, April 21, 2015

Huenda 800 waliangamia baharini 


Mashua ya wahamiaji iliyozama.

Federica Mogherini
Umoja wa Mataifa unasema unahofia kuwa huenda watu 800 walifariki siku ya Jumapili, pale mashua waliyokuwa wakilitumia kuvuka bahari ya Mediterenean ilipozama karibu na Libya.
Shirika la Umoja wa mataifa linalowashughulikia wakimbizi UNHCR, limekuwa likizungumza na manusura baada ya kuwasili katika kisiwa cha Sicily mapema leo Jumanne.
Federica MogheriniMkuu wa sera kwenye Muungano wa Ulaya Federica Mogherini anasema kuwa pana haja ya kuwepo hatua za haraka ili kushughulikia suala kuhusu wahamiaji katika bahari ya Mediterranean, huku akizindua mikakati kumi ya mpango wa kutanzua vifo vya wahamiaji.
Mogherini, anasema kuwa mipango hiyo ni hatua kubwa ya kuzuia kupotea kwa maisha ya watu. Majukumu ya muungano huo ni kuzidisha operesheni ya uokozi, pamoja na mipango mipya ya kuharibu mashua zinazotumiwa na walanguzi wa binadamu wanaowavusha watu baharini.CHANZO:BBC (Muro)

No comments:

Post a Comment