TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, April 13, 2015

African Sports yakwapua beki wa Simba kujipa makali 

AFRICAN Sports iliyopanda daraja kucheza Ligi Kuu Bara msimu ujao, imeanza usajili kwa kumnasa beki wa zamani wa Simba, Hassan Khatib na winga wa Kurugenzi ya Daraja la Kwanza, Jafar Kibaya.
Akizungumza na Mwanaspoti, Meneja wa timu hiyo, Abdulhalim Hemed, alisema wapo kwenye hatua nzuri ya mazungumzo na wachezaji hao ambao wana sifa za mahitaji ya timu yao.
"Hao ni wachezaji kati ya watano ambao tuna uhakika wa kumalizana nao, kwani wengine tunaogopa kuwaweka wazi tunahofia hujuma za timu zenye fedha zao kwani wakisikia tu tunawasajili watataka wawasajili kwenye timu zao," alisema.(P.T)
Baada ya Khatibu kutemwa Simba , alijiunga na Friends Rangers ya Ligi Daraja la Kwanza , iliyopo chini ya katibu Herry Mzozo, anayeaminika kuibua wachezaji wengi wanaokipiga Ligi Kuu Bara, akiwemo Salum Abubakar 'Sure Boy' wa Azam FC.
Mbali na hilo alisema hawana mpango wa kuwasajili wachezaji wa Simba, Yanga na Azam FC kwa sababu hawataki ugomvi na timu hizo zenye sifa za kutumia fedha nyingi katika usajili isipokuwa wanaangazia macho yao katika timu ya Mtibwa Sugar.
"Hatuna haja na wachezaji wa Simba, Yanga na Azam FC, kwani timu yetu haina uwezo wa kushindana nao kifedha ili tutasajili wasio na majina makubwa, lakini wenye uchu wa mafanikio yao pamoja na timu kwa ujumla," alisema.
Mbali na hilo pia alisema wapo kwenye harakati ya kusaka wadhamini ambao ndio watakaowawezesha kukamilisha mpango wao wa usajili wa wachezaji ambao wamewaona ndio watakaoisaidia timu kufika pazuri.
"Kuna mambo mengi yanaendelea katika kikosi chetu ya kuhakikisha tunaanza ligi msimu ujao timu ikiwa imejipanga kwa ajili ya kufanya kazi na si vinginevyo," alisema.
http://www.mwanaspoti.co.tz/

No comments:

Post a Comment