TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, April 13, 2015

JK awananga wanasiasa wanaotumia mgongo wa dini 


Rais Jakaya Kikwete akiwa kwenye picha ya pamoja na maaskofu wa kanisa la Katoliki mara baada ya kumalizika kwa ibada ya kumweka wakfu askofu mpya wa jimbo katoliki Shinyanga, Mhashamau baba Askofu Leberatus Sangu
Shinyanga. Rais Jakaya Kikwete amewataka viongozi wa dini nchini kutowaonea haya viongozi wa kisiasa wanaotaka kugeuza nyumba za ibada kuwa majukwaa ya kufanyia siasa kwa kuwa hali hiyo inaweza kusababisha vita ya kidini au waumini kwa waumini.
Rais Kikwete alisema hayo jana wakati wa ibada ya kuwekwa wakfu na kusimikwa rasmi, askofu mpya wa Jimbo la Shinyanga, Liberatus Sangu katika Kanisa la Mama Mwenye Huruma, Parokia ya Ngokolo, Shinyanga.
Aliwataka viongozi hao kuhakikisha makanisa na misikiti inabaki kuwa sehemu ya ibada na usuluhishi na iwapo watashindwa, inaweza kusababisha makundi na mapigano.
"Katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu, wanasiasa wengi wanapenda kutumia tofauti za rangi, ukabila na dini nawaomba msiruhusu mambo hayo ni hatari kwa Taifa, endeleeni kukemea jambo lolote ambalo mnaona linakwenda tofauti."
Rais Kikwete pia alizungumzia mauaji ya vikongwe na albino huku alimtaka Askofu Sangu na maaskofu wengine kuongeza bidii kuwalea waumini wao katika imani, ili waachane na vitendo vya kishirikina ambavyo ndivyo chanzo cha mauaji yao.
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo alimsimika rasmi Askofu Sangu na kumkabidhi fimbo ya kichungaji huku akimtaka kuhakikisha anafanya kazi kwa kushirikiana na viongozi wengine na kumtakia heri na baraka katika muda wake wote wa kitume.
Kwa upande wake, Askofu Sangu alisema kazi kubwa iliyo mbele yake ni kuhakikisha analinda na kustawisha mema yote yaliyoachwa na waliomtangulia.
"Nitashirikiana na viongozi wenzangu pamoja na Serikali katika masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na kukemea mauaji ya vikongwe na albino. Sala zenu ndizo ambazo zimesababisha mimi nikateuliwa na baba mtakatifu kuwa askofu na leo hii nimesimikwa rasmi kuanza kazi katika jimbo hili la Shinyanga, nawaomba waumini wote tushirikiane kwa pamoja katika kazi hii."
Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa alimtaka Askofu Sangu kuchunga kondoo wake aliokabidhiwa kwani wanahitaji upendo pamoja na kushirikiana vizuri na wasaidizi wake katika kuleta maendeleo na kuwalea waumini kiimani.
Ibada hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwamo waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa.CHANZO: MWANANCHI (Muro)

No comments:

Post a Comment