TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, April 20, 2015

Semina ya Texas Karate Black Belts yafanyika Houston, Texas 



Texas Black Belts club Seminar , imeandaliwa na Sensei Ramon Veras, Dan 7, Okinawa Goju Ryu Kyokai, mjini Houston, Texas tarehe 19 April, 2015. Pia ni sehemu moja ya maandalizi na marekebisho ya mbinu na ufundi wa vipande tofauti katika mfumo mzima wa Sanaa na tayari kwa baadhi ya washiriki kwa msafara wa kwenda kwenye chimbuko la Karate huko Okinawa, Japan.
Sensei Rumadha Fundi, ni mmoja ya wawakilishi wa Goju Ryu Jundokan, atayoiwakilisha Tanzania kwenye msafara huo..
Baada ya takriban miaka 23 sasa, sensei Rumadha Fundi "Romi", anarejea tena chini Japan kama alivyofanya mwezi May mwaka 1992. Safari hiyo ya mwezi June kwenda Naha City, Okinawa kwa njia ya Los Angeles, Tokyo na hatimaye Naha City, Okinawa.
Sensei Rumadha amepewa mwaliko kama mwakilishi wa Jundokan Tanzania, kwa niaba ya kuwa mteule na mwakilishi wa chama hicho cha mtindo wa Okinawa Goju Ryu, chini ya rais wake ambaye ni mtoto wa Eiichi Miyazato mwanzilishi wa chama hicho Sensei Yoshihiro Miyazato "Kancho", na hatimae kupewa jukumu la kusambaza Jundokan nchini kote akiwa"Tanzania Chief Instructor " na kupewa madaraka ya kutowa idhini na mikanda ya wawakilishi wa Jundokan nchini Tanzania na utambulisho wa kutowa vyeti ( Dan Certificate) kutoka, Naha, Okinawa.
Sensei Rumadha anashikilia Dan 6 toka Tanzania Karate-do Federation, na Dan 3 toka Jundokan Kyokai.Lengo na madhumuni ya sensei Rumadha ni kusambaza ufanisi wa Goju Ryu na mbinu za "Muchimi" ni undani halisi wa utumiaji mbinu kifasaha na kitamaduni kama ifanyavyo huko Okinawa, Japan.
Sensei Rumadha, atafanya mazoezi katika dojo ambayo mwalimu wake yeye Sensei Bomani na Master Morio Higaonna walikuwa wanafunzi hapo miaka 45-50 iliyopita. Pia Sensei Rumadha, atatembelea sehemu zenye historia ya mwanzao wa Karate na makaburi ya waanzilishi wa Sanaa na makumbusho ya Karate na vitongoji vyake kama, Naha, Shuri na Tomari, Okinawa , Japan.
Nia na madhumuni makubwa ni kutaka kuiendeleza Goju Ryu Karate Tanzania na hatimae kuwa na walimu wenye utambulisho huko, Okinawa, Japan na kuleta maendeleo na maslahi ya kimaisha kama mwalimu wa Karate.
Pia Sensei Rumadha alisema " Tapenda kubadilisha mfumo wa jinsi Goju Ryu inafundishwa Tanzania. Tawapa mwaliko wanafunzi wote wenye nia ya mafanikio na utambulisho toka Okinawa, kuwa chini ya uongozi wangu na kuendeleza utamaduni wa Goju Ryu. Goju Ryu ina matawi mengi na uongozi tofauti, mimi napendelea kuwa na shina la Okinawa Goju Ryu Karate – do, lililowekwa na waanzilishi wa mtindo huo; lengo ni kuwa na Goju Ryu halisi na sio mabadiliko", alisema Sensei Rumaha.(Muro)

No comments:

Post a Comment