Wanajeshi wanamaji wanne wauawa Marekani

Rais wa Marekani Barack Obama
Mtu 
mwenye silaha amewaua askari wanne wa jeshi la wanamajiwa Marekani 
katika shambulio lililofanywa kwenye majengo mawili ya jeshi hilo katika
 mji wa Chattanooga, Tennessee. Wanajeshi hao wote waliuawa katika jengo
 moja. Maafisa nchini humo wameyaita mauaji hayo kuwa ni Shambulio la 
ndani. Shirika la Upelelezi la Marekani FBI linalochunguza mauaji hayo, 
limesema halijajua bado kilichosababisha shambulio hilo.
Kufuatia tukio hilo maeneo kadhaa yamefungwa zikiwamo hospitali na shule ili kuchukua tahadhari.BBC
        
"Ni 
mazingira ya kusikitisha kwa watu ambao wametumikia taifa kwa moyo 
wote,kuuawa katika mfumo huu inasikitisha. Wakati maandalizi ya 
mawasiliano na familia za wanajeshi hawa yakifanyika, naomba wafahamu 
kuwa nazungumza kwa niaba ya raia wote wa Marakani kuelezea masikitiko 
yangu na kuwahakikishia kuwa tupo nao katika mazingira haya magumu".
Naye Meya
 wa jiji la Chattanooga Andy Berke alisema muuaji aliuawa na polisi. Pia
 ofisa wa polisi pamoja na watu wengine wamejeruhiwa.
"tunafahamu
 kuwa kuna watu wanne waliouawa. Tunafahamu kuwa muuaji pia aliuawa 
katika eneo la tukio na pia afisa wa polisi mmoja wa Chattanooga 
amepigwa risasi kwenye kifundo cha mguu na anatibiwa vilevile pale 
Arlanga, pia kulikuwa na watu wengine waliopigwa risasi na wametibiwa
Mwanasheria mkuu wa jimbo la Tennessee, Bill Kilden, ameyaelezea mauaji hayo kama ugaidi wa ndani
No comments:
Post a Comment