TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Sunday, July 12, 2015

MKUTANO MKUU CCM WAMALIZIKA DODOMA 


 Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akihutubia wajumbe wa mkutano Mkuu wa CCM kwenye ukumbi mpya wa mikutano wa CCM ujulikanao kwa jina la Dodoma Convention Center.

 Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiinua mikono juu ya mgombea wa urais kupitia CCM John Pombe Magufuli mara baada ya kumtangaza rasmi.

 Baadhi ya wajumbe wakifuatilia kwa makini hotuba za viongozi wao

Mke wa Rais ya Jamhuti ya Muungano Tanzania Mama Salama Kikwete (kulia) akicheza muziki pamoja na mke wa mgombea uraisi kupitia CCM ,Janneth Magufuli

 Mgobea wa nafasi ya Urais kupitia CCM Mhe.John Magufuli akihutubia wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM na kuwataka kuendelea kushikamana .

 Kila mtu alionekana mwenye furaha.

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akimsalimu mgombea wa nafasi ya urais kupitia CCM

 Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwainua mikono juu mgombea wa nafasi ya Urais John Magufuli na mgombea mwenza Mhe. Samia Suluhu Hassan

 Picha ya pamoja na meza kuu.

 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Mhe.John Pombe Magufulu pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakiwasalimia wananchi waliojitokeza kwenye uwanja wa  Jamhuri mjini Dodoma

 Mhe. Magufuli akiwapa mikono wananchi waliojitokeza kwa wingi kuja kumsalimia na kumuona mgombea huyo wa CCM.

 Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasalimu wananchi wa Dodoma kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma

Mgombea wa Urais wa CCM Mhe. John Magufuli akizungumza wakazi wa Dodoma ikiwa sehemu yake ya kwanza  kujitambulisha kwa wananchi mara baada ya kutangazwa.

No comments:

Post a Comment