TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, July 16, 2015

CHAMA CHA MADEREVA TANZANIA CHATOA TAMKO


Kaimu Katibu Mkuu wa Chama Cha Madereva, Rashid Saleh (kushoto) akitoa tamko hilo. Kulia ni mtunza hazina wa Chama hicho, Ramadhan Seleman.

....akihojiwa na waandishi wa habari.
CHAMA cha Madereva Tanzania,  kimetoa tamko rasmi juu ya marekebisho ya mikataba yao, huku kikilalamikia kile kilichoitwa... “ukiukwaji wa makubaliano”.(P.T)
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar mapema leo, Kaimu Katibu Mkuu ambaye pia ni msemaji wa chama hicho, Rashid Saleh alisema miongoni mwa mambo na makubaliano ambayo anadai yamekiukwa ni pamoja na ucheleweshwaji wa posho, ambazo kwa mujibu wa mkataba zilitakiwa kuanza kutolewa Julai mosi mwaka huu,  jambo ambalo halijatekelezwa.
Alisema, kwa sasa wanafanya taratibu zote muhimu kwa lengo la kujua hatma yao huku madeva wakitishia kugoma tena endapo haki juu ya mkataba huo hazitafuatwa kulingana na makubaliano.
Hata hivyo, msemaji huyo alilalamikia uzembe Wizara ya Kazi, Ajira na Vijana pamoja na Mamlaka ya Usafirishaji wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra) wa kushindwa kusimamia waliyoiita “tume ya uchunguzi” ambayo imeonekana kuchelewa kutimiza jukumu hilo.

No comments:

Post a Comment