Akon kuleta umeme Afrika

Muimbaji 
wa miondoko ya R&b anayeongoza katika chati za juu za muziki huo 
duniani 'Akon' ameamua kutumia tasnia yake ya muziki kukabiliana na 
maendeleo endelevu ya watu wa barani Afrika.
Nyota 
huyo wa R & B anazindua mpango maalumu wa mafunzo unaoitwa "Akon 
Angaza Afrika" ambao una lengo la kutumia nguvu ya jua kuzalisha umeme 
huku akiwa na matumaini ya kuwafikia watu milioni 600 barani wa Afrika.
Ufunguzi 
wa huo umefanyika mjini mkuu wa Bamako nchini Mali, baadaye mafunzo hayo
 yatafundisha kwa wadau wa mradi huo jinsi ya kutunza mifumo ya nishati 
hiyo inayoendeshwa kwa nguvu ya jua.
Samba 
Bathily ambaye ni mwanzilishi msaidizi wa mradi huo, anasema jua na 
teknolojia hiyo ya ubunifu itasaidia kuleta umeme katika nyumba na 
kwenye jamii kwa ujumla.
Kwa sasa anasema kuwa wanaimarisha utaalamu wa Kiafrika na kwamba hilo ni lengo lao.
Ameelezea
 sababu ya kuwekeza zaidi kwenye nishatiya umeme kwamba ni moja ya njia 
ya kutoa fursa za kiuchumi na huduma za kijamii kwa bara la Afrika 
ambalo sehemu kubwa ni giza kutokana na ukosefu wa Nishati.
No comments:
Post a Comment