TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, July 22, 2015

Haya ndio maamuzi ambayo Rafael Van der Vaart anajutia kwenye maisha yake ya soka

rafael-van-der-vaa_1996045c
Kiungo wa kimataifa wa kiholanzi Rafael van der vaart ambaye amewahi kuitumikia Tottenham Hotspurs  kuanzia 2010-2012 akitokea katika klabu ya Real Madrid ya Hispania uhamisho ulioshangaza wengi kwa kiungo huyo kujiunga White Hart Lane.
rafael-van-der-vaart
Van der Vaart alikuwa kipenzi cha mashabiki wa Spurs na alifanikiwa kuifungia magoli 28 katika mechi 78 na kuisaidia timu kufika hatua ya robo fainali ya Klabu Bingwa Ulaya chini ya kocha Harry Redknapp wakati huo kabla ya kufukuzwa na nafasi yake kuchukuliwa na kocha Villas Boas.
rafael-vaart
Baada ya kuhama Spurs 2012 alijiunga na Hamburger SV ya Ujerumani kabla ya 2015 kurudi Hispania kwa mara nyingine tena ila katika klabu ya Real Betis, hadi leo hii Van der Vaart anasikitikia maamuzi yake ya kuhama Tottenham Spurs.
hlad8zk
Van der Vaart akitambulishwa Real Betis 2015
“Yalikuwa maamuzi binafsi ila wakati alipokuja Villas Boas aliniambia mimi sio chaguo lake la kwanza, huwezi kuamini nilikuwa nimecheza misimu miwili pale… kitu ambacho kilikuwa kigeni kwangu, nikaona bora kuondoka”>>>Van derVaart
“Ulikuwa ni uamuzi wa kijinga katika maisha yangu ya soka kuhama Tottenham, kiukweli najutia nilikuwa na misimu miwili mizuri katika maisha yangu ya soka”>>>Van der Vaart

No comments:

Post a Comment