TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, July 22, 2015

Hata South Africa wana matatizo yao pia, mvulana apoteza maisha baada ya mchezo huu kwenda vibaya!

DAANG
Loyiso kijana wa miaka 19 ameweka headlines kubwa sana jijini Johannesburg South Africa baada ya tukio la janga la treni kutokea mjini hapo.
Kijana huyo aliyekuwa kwenye kipindi cha mitihani alifariki siku ya jana baada ya kuthubutu kucheza mchezo wa kurukaruka ndani na nje ya treni iliyokuwa kwenye spidi kali, mchezo unao hatarisha maisha.
Train SA1
Loyiso alikuwa njiani kuelekea shule wakati mchezo huo ulipogeuka kuwa tukio la kutisha, baadhi ya abiria waliokuepo kwenye treni hiyo walisema…
>>> “alikuwa anarukaruka ndani na nje ya treni hii na kwa bahati mbaya aliteleza na kuingia katikati ya reli za treni tukiwa tunakaribia kituo cha Chiawelo Railway Station”.<<< 
TRAIN SA2
>>>walikuwa kikundi…kikundi cha vijana waliokuwa wanacheza mchezo huu, lakini kwa bahati mbaya huyo mmoja aliteleza na kuingia chini ya reli ya treni na kichwa chake kilisagwa. Ni tukio la kutisha sana na linavunja moyo.<<<
Vyombo vya kulinda usalama kwenye kituo cha Chiawelo Railway Station vimekuwa vikijaribu kupambana na tatizo la mchezo huu kwa muda mrefu sana kwani limekuwa tishio kwa jamii. Tukio hili limewaacha ndugu, jamaa, marafiki pamoja na wanafunzi wengi na masikitiko makubwa.

No comments:

Post a Comment