TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, September 10, 2014

TAMISEMI YATAKA KUONGEZA ZAIDI KIWANGO CHA TAHADHARI YA UGONJWA WA EBOLA.

 Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk Godfrey Mtei akipokea zawadi ya saa ya ukutani kutoka kwa Waziri wa Tamisemi, Hawa Ghasia, juzi mjini hapa.
 picha ya pamoja .
 Picha ya pamoja baadhi ya waganga wakuu wa wilaya na mikoa wakiwa na Mgeni rasmi , Waziri wa Tamisemi, Hawa Ghasia.
 Waziri wa Tamisemi, Hawa Ghasia akikambishi zawadi ya saa ya ukutani Mganga Mkuu wa Serikali,Dk Donan Mmbando,saa hiyo iliyolewa na Taasisi ya Lab Eguip Limited.
 Baadhi ya waganga wakuu wa wilaya na Mikoa ya Tanzania Bara wakisiliza hotuba ya Waziri wa Tamisemi, Hawa Ghasia ( hayupo pichani).
 Dk Frida Mokiti ( kushoto) akibadilishana mawazo na mwezake wakati wa mapumziko
Waziri wa Tamisemi, Hawa Ghasia, akiwa na Mganga Mkuu wa Serikali, Dk Donan Mmbando , baada ya waziri kufungua mkutano.

Na John Nditi, Morogoro
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),Hawa Ghasia, amewaagiza  Waganga Wakuu wa Mikoa , na Halmashauri za wilaya nchini kuongeza zaidi kiwango cha kuchukua tahadhari katika kukabiliana na magonjwa ya mlipuko ukiwemo wa Ebola.
Waziri Ghasia alitoa agizo hilo jana mjini hapa wakati wa  hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa Waganga wakuu wa mikoa, Halmashauri za wilaya na wakurugenzi wa Hospitali za rufaa kutoka mikoa yote ya Tanzania bara.
Kwa mujibu wa Waziri huyo kuwa, hapa nchini ugonjwa huo  haujathibitika kuingia na Serikali imechukua tahadhari zote kuhakikisha kuwa ugonjwa huo hauingii  nchini na endapo utathibikika kuingia uweze kudhibitiwa kikamilifu.
Hata hivyo alisema , mwaka huu kumekuwepo na matukio ya hapa nchini na nje ya nchi yaliyotufanya tuongeze zaidi kiwango cha tahadhari , na tukio la kwanza ni la mlipuko wa ugonjwa wa Dengue , ambao uliwapata wagonjwa 1,384 kote nchini, na kusababisha vifo vya watu wanne , sehemu kubwa ya wagonjwa walikuwa ni wa Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Waziri huyo , tukio la pili ni la ugonjwa wa ebola ,ambao kwanza ulianzia nchi za Afrika Magharibi,  na kati ya Machi hadi Agosti mwaka huu , watu 3,069 waliungua ugonjwa huo.
Hivyo  hadi kufikia Agosti 28, mwaka huu ,ugonjwa huo umeua watu 1,552 na hivi karibuni umeingia nchi ya Congo DRC na kufikia mwishoni mwa mwezi uliopita watu 24 wameripitiwa kuugua .
“ Ni matumaini yangu kuwa katika mkutano huu  , suala la magonjwa ya mlipuko kama haya yatajadilikwa kikamilifu ili kila mmoja wenu awe katika tahadhari kubwa” alisisitiza Waziri Ghasia
Hata hivyo , Waziri Ghasia alitumia fursa hiyo kutoa shukrani za Serikali ya Tanzania kwa Watu wa Marekani kupitia Shirika lao la CDC na Shirika la Afya Duniani kwa kutoa vifaa na vifaa tiba kwa ajili ya kuzuia maambukizi ya ugonjwa huo wa ebola.
Mbali na tahadhari ya magonjwa ya mlipuko, Waziri Ghasia alisema , katika ziara zake sehemu mbalimbali hapa nchini ameshuhudia juhudi zinazofanywa na wadau katika kuboresha upatikanaji  na utoaji wa huduma za afya na ustawi wa jamii.
Kwa mujibu wa Waziri huyo kuwa juhudi hizo ni  kujenga vituo vipya vya huduma za afya , kukarabatiwa vituo ambavyo havipo katika hali nzuri  kuongeza watumishi na upatikanaji wa dawa, vifaa tiba na kuimalisha utaratibu wa kukusanya mapato katika vituo.
Pia ulimalishaji wa utoaji wa huduma kwa makundi maalumu hususan , wanawake wajawazito, watoto chini ya miaka mitano na  wazee  katika baadhi ya maeneo husika.
Hata hivyo alisema ,kutokana na juhudi hizo, malalamiko kuhusu uhaba wa dawa na vitendo vya rushwa yamepungua katika maeneo ambako juhudi hizo zimekwishafanyika.
“ Nimefurahishwa  na kasi ya ujenzi mpya wa Zahanati na Vituo vya Afya .... juhudi hizi zinapaswa kupongezwa  kwa vile ni utekeleaji wa Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (MMAM)” alisema Waziri Ghasia .
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Serikali , Dk Donan Mmbando, kabla ya kumkaribisha waziri , alisema lengo la mkutano huo ni kujadili masuala muhimu yanayolenga kuboresha huduma za afya na ustawi wa jamii hapa nchini na pia kuainisha changamoto mbalimbali zinazowakabili watumishi wa wizara hiyo.
Hata hivyo alitumia fursa hiyo kuwakumbusha wataalamu hao wa sekta ya afya kujipanga kukabiliana magonjwa ya mlipuko ukiwemo wa ebola na kutenga maeneo maalumu kwa ajili ya kutolea huduma endapo kutakuwa na udhibitisho wa dalili za wagonjwa katika maeneo yao.
Pamoja na kuzungumzia changamoto zilizopo ikiwemo ya ya  usimamizi wa utendaji bora na uboreshaji wa  mazingira ya kazi na y a watumishi , pia aliwataka wataalamu wao kuangalia namna ya kukabiliana na ongezeko la magonjwa yasiyoambukizwa ukiwemo wa saratani.
Kwa mujibu wa Manga Mkuu wa Serikali, kuwa vituo vingi vya Afya vilijengwa kwa kuangalia upande mmoja wa kukabiliana na magonjwa ya kuambukiza na kusahau mengine yasiyoambukizwa na kwamba hatua zaidi zinapaswa kuchukuliwa ili kukabiliana nayo na kutaka yaingizwe kwenye mpango kazi wa mwaka 2016

No comments:

Post a Comment