Hong Kong bado hali tete

Raia wa Hong Kong wakivurumushiwa moshi
Makumi 
kwa mamia ya waandamanaji wa Hong Kong wanaendelea na maandamano yao kwa
 siku nyingine tena baada ya kudhoofisha maeneo muhimu ya jiji hilo 
wakati wa mchana. Waandamanaji hao sasa wanamtaka Mkuu wa utawala wa 
Hong Kong Leung Chun-Ying ajiuzulu..
Wakati 
huo huo Marekani imesema inafuatilia kwa karibu kinachoendelea Hong Kong
 na imeutaka utawala kuchukua hatua. Katika mkutano wa wanahabari 
msemaji wa Ikulu ya Marekani Josh Earnest amesema Marekani inaunga mkono
 matakwa ya watu wa Hong Kong.
"Duniani 
kote, na hii ni kweli katika Hong Kong na maeneo mengine, Marekani 
inaunga mkono kimataifa, uhuru, kama vile uhuru wa kukutana kwa amani na
 uhuru wa kujieleza. Marekani inautaka utawala wa Hong Kong kuchukua 
hatua, na kwa upande wa waandamanaji kutoa maoni yao kwa amani"BBC
No comments:
Post a Comment