MWANDISHI WA HABARI ITV/RADIO ONE AZIMIA KWA KIPIGO CHA POLISI
Mwandishi wa habari Badi akilia baada ya kushambuliwa na Polisi,huyu ni moja ya waandishi walioshambuliwa

Kuna 
taarifa kuwa mwaandishi wa habari wa IPP Media kapigwa na jeshi la 
polisi alipokuwa ameenda kuripoti matukio yaliyokuwa yanaendelea baada 
ya mwenyekiti wa CHADEMA Mhe, Mbowe alipoenda kuitikia wito wa jeshi 
hilo la polisi.
Habari 
zinasema kuwa baada ya Mbowe na wanasheria kuingia ndani polisi walianza
 kupiga kila aliyekuwa eneo la tukio bila kujali ni nani ndipo 
alipojikuta mwandishi huyo akipigwa mpaka kupoteza fahamu...(MC)
Imeelezwa
 kuwa waandishi wengi wa habari wameumia vibaya kutokana na kukimbizwa 
na mbwa wa polisi huku wengine wakiumwa na mbwa hao.
Waandishi
 wa habari wameshindwa kutimiza wajibu wao kwa kuzuiwa na polisi ambao 
wameshindwa kutambua uwepo wa waandishi wa habari,Je Uhuru wa vyombo vya
 habari uko wapi Tanzania? na kama waandishi wa habari wameanza kuumizwa
 mapemaa kabisa kabla hata kampeni za uchaguzi hazijaanza,Sijui uchaguzi
 ukifika hali itakuwaje!!
Ikumbukwe
 kuwa Mwaka jana mwandishi wa habari Daud Mwangosi aliuawa kikatili kwa 
amri ya RPC (Kamuhanda) wa Iringa wa wakati huo ambaye baada ya kutimiza
 azima yake hiyo alipandishwa cheo.
Mami ya 
watu leo wamejitokeza kumsindikiza Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha 
Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, baada ya kuhitajiwa 
kufika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi nchini, jijini Dar es Salaam 
kuhusiana na kauli yake aliyotoa Septemba 14 mwaka huu,juu ya kuitisha 
maandamano nchi nzima kupinga kuendelea kwa Bunge Maalum la Katiba.
Kilichofuata
 ni polisi kuamuru watu wote waondoke eneo hilo kwa umbali wa mita 200 
ambapo walikimbizwa na mbwa wa polisi na kusababisha wengi wao waumie na
 kupoteza vitu vyao mbalimbali, hususani wanahabari ambao baadhi yao 
waliumia na kupoteza zana zao za kazi.
CHANZO; GPL
No comments:
Post a Comment