ANAYEDAIWA KUWA TAPELI WA AJIRA ANASWA

Stori: Chande Abdallah na Deogratius Mongela
YAHAYA unaishi
 wapi? Jamaa mmoja anayetumia majina ya Baraka, Muba au Martha Peter 
amenaswa kwa kujipatia pesa kiudanganyifu akijifanya Ofisa wa Bodi ya 
Mikopo wa Chuo cha Ardhi kilichopo jijini Dar.
Tapeli anayetumia majina ya Baraka, Muba au Martha Peter.
Tukio 
hilo lilitokea  Septemba 19 mwaka huu katika Kituo cha Afya cha Kimara 
baada ya tapeli huyo kumlaghai dada mmoja aitwaye Wema Raymond wakutane 
hapo kwa ajili ya vipimo vya ukimwi vilivyotakiwa kuambatanishwa katika 
fomu ya kuomba nafasi ya kazi ambayo awali dada huyo alidai kupatiwa na 
tapeli huyo.(P.T)
Akizungumza
 na waandishi wetu, Wema alisema alimfahamu tapeli huyo kupitia kwa 
rafiki yake aliyemtaja kwa jina la Rebecca, ambaye naye awali alipigiwa 
simu na mtu huyohuyo akimtaka kimapenzi.
Wema 
alisema kuwa rafiki yake alimkatalia tapeli huyo, lakini siku chache 
baadaye alimpigia tena akimwambia kulikuwa na nafasi ya kazi katika Chuo
 cha Ardhi hivyo anamhitaji yeye kwa ajili ya nafasi hiyo.
“Kwa 
sababu Rebecca ana kazi yake tayari aliamua kunitaarifu mimi kwa kuwa 
anajua natafuta kazi,” alisema Wema.Alisema alikutana na jamaa huyo 
ndani ya Chuo cha Ardhi na kupatiwa fomu aliyoelekezwa kujaza kisha 
akatakiwa kutoa shilingi 280,000 kama malipo ya fomu hiyo na gharama za 
mafunzo ya siku tatu ya vitendo kuhusu kazi, fedha ambazo hakuwa nazo 
kwa muda huo na kulazimika kumuomba rafiki yake Rebecca amsaidie.

Wema Raymond aliyetapeliwa na tapeli huyo anayefahamika kwa jina la Baraka au 'Muba'.
“Baada ya
 kumaliza mazungumzo pale chuoni akanisindikiza hadi nje, lakini cha 
kushangaza pale mlangoni nikamuona anampatia mmoja wa walinzi hela, 
nikamuuliza kwa nini aliwapa hela, akasema eti watu wengi wanaitaka 
nafasi ile wakiwemo walinzi hao, hivyo alikuwa akiwapoza wasimsemee kwa 
kunitafutia mimi kazi isije akafukuzwa kazi,” alisimulia Wema na 
kuongeza kuwa alitakiwa kesho yake kupima VVU ili vipimo hivyo 
viambatanishwe kwenye barua yake ya maombi.
Katika 
Kituo cha Afya Kimara, alikutana tena na tapeli wake, aliyeonekana 
kuwasalimia madaktari na manesi kana kwamba wanajuana kisha akaingia kwa
 dokta na kuzungumza naye.Baada ya muda tapeli huyo alitoka nje  kisha 
akamwambie Wema aingie kwa daktari kwa ajili ya kujaziwa fomu hizo 
kienyeji bila kupimwa maambukizi ya ukimwi.
“Nikiwa 
ndani machale yalinicheza, ikibidi nimuulize yule daktari kama anajuana 
na yule jamaa, daktari akasema kwamba hawafahamiani hata kidogo jambo 
lililonishtua. “Nikamnong’oneza kuwa nahisi kutapeliwa, akaniambia 
nikakae naye nikijifanya namuongelesha huku yeye akizunguka kwa mlango 
wa nyuma na kuwaita mapolisi.

Kamanda Suleiman Kova.
“Katika 
upekuzi alikutwa na zile pesa zangu za jana zikiwa kwenye simu yake na 
shilingi 90,000 akiwa nazo mfukoni huku akionekana kutumia simu yenye 
jina la Martha Peter ambalo mwenyewe alikiri kuwa alikuwa akinitapeli.”
“Polisi 
walichukua maelezo yangu na kufungua jalada RB/4969/2014 KUJIPATIA PESA 
KIUDANGANYIFU kisha wakaniambia nifike kesho yake,” alisema Wema na 
kuongeza kuwa siku ya pili alipofika kituoni hapo aliwakuta watu wengine
 waliodai kutapeliwa na jamaa huyo kwa majina tofauti na walipopiga 
hesabu fedha alizowatapeli kwa pamoja zilifikia sh.1,435,000.
No comments:
Post a Comment