JK ATAKA MSAADA ESRF KUONDOA UMASKINI KWENYE UCHUMI UNAOKUA
Mkurugenzi
 Mtendaji wa Taasisi Huru ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dk. 
Hoseana Lunogelo akisalimiana na Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa 
Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP)
 nchini , Alvaro Rodriguez nje ya ukumbi wa mikutano kabla ya mgeni 
rasmi kuwasili kwenye mkutano mkubwa wa tatu wa ESRF unaozungumzia 
ukuaji wa uchumi kwa kutumia fursa zilizopo na maendeleo yanayogusa 
jamii uliofanyika jana jijini Dar katika hoteli ya Hyatt Regency, 
Kilimanjaro.(Picha zote na Zainul Mzige wa MOblog)
Na Mwandishi wetu
RAIS
 Jakaya Kikwete amewataka nguli wa masuala ya uchumi na maendeleo ya 
binadamu kuisaidia serikali kufanikisha azma yake ya maendeleo kwa 
wananchi hasa ikizingatiwa kwamba zipo raslimali za kutosha, uchumi 
unakua lakini umaskini haupungui.
Rais
 alisema hayo jana wakati akifungua mkutano mkubwa wa tatu wa Taasisi 
Huru ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF) unaozungumzia ukuaji wa uchumi
 kwa kutumia fursa zilizopo na maendeleo yanayogusa jamii uliofanyika 
hoteli ya Hyatt Regency, Kilimanjaro.
Katika
 hotuba yake kwa wataalamu nguli hao ambao wanaangalia athari za kisera 
na kutoa ushauri katika masuala ya maendeleo yenye kulenga kunufaisha 
jamii, alisema katika miaka 10 iliyopita uchumi wetu umekua ukikua kwa 
kasi lakini hali hiyo haikuweza kusaidia kupunguza umaskini kama 
ulivyolengwa na serikali...(MC)
Alisema
 moja ya malengo ya millennia yalikuwa ifikapo mwaka wa kesho hali ya 
umaskini ipunguzwe angalua nusu yake, kwa kuongeza pato la mtu binafsi 
lakini hali sivyo ilivyo.
Rais
 ambaye alitumia muda mwingi kueleza maendeleo ya kiuchumi yaliyofikiwa 
katika hatua ya kuifikisha nchi hii miongoni mwa mataifa yenye kipato 
cha kati ifikapo mwaka 2025, alisema zinatakiwa juhudi kubwa ili kuondoa
 umaskini wa kipato kwa mtu mmoja mmoja.
Mwenyekiti
 wa Bodi ya ESRF, Philemon Luhanjo (kushoto) akiteta jambo na Mratibu 
Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la 
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez nje ya 
ukumbi wa mikutano kwenye hoteli ya Hyatt Regency, Kilimanjaro.
“Pamoja
 na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika ustawi wa jamii kama 
uandikishaji wa watoto shule, uzazi na upunguzaji wa vifo vya watoto, 
taifa bado linakabiliwa na changamoto kubwa ya ubora wa elimu, 
upunguzaji wa vifo kwa wanawake wazazi na utapiamlo” alisema Rais 
Kikwete.
Alisema
 kwa kuangalia takwimu hizo katika jamii na ukuaji wa uchumi ni dhahiri 
kwamba taifa letu ili kufikia malengo yake kuna mambo mengi yanatakiwa 
kufanyiwa kazi na kuamini kwamba wataalamu hao katika mada zao 
mbalimbali watakazojadiliana watatoka na kitu cha maana kuisaidia 
serikali kupata mwelekeo sahihi wa kufikia taifa lenye kipato cha kati 
ifikapo mwaka 2025.
Dira
 ya maendeleo ya mwaka 2025 ambayo inayotaka kuifanya Tanzania kuwa nchi
 ya kipato cha kati yenye maisha bora, utawala bora na uchumi wenye 
ushindani miongoni mwa mambo machache yenye upeo wa juu yaliyomo katika 
dira hiyo ndiyo yanayotumika kujadili na hatimaye kuipa serikali 
majawabu ya mambo muhimu yanayotikisa safari ya kuelekea huko.
Ili
 kufika huko kwa mujibu wa Rais Kikwete viashiria kadhaa vitaonekana 
ikiwa ni pamoja na kushuka kwa mchango wa kilimo kwa pato la taifa na 
ajira, kukua kwa sekta ya kisasa ya viwanda na huduma kwa uchumi, kukua 
kwa miji na mabadiliko katika vizazi na vifo ambapo taifa linaondoka 
katika vifo na uzazi wa fujo na kuwa na vizazi vidogo na vifo kidogo 
kutokana na kukua kwa elimu na huduma za afya.
Mkurugenzi
 Mtendaji wa ESRF Dk. Hoseana Lunogelo (kushoto) akiongozana na Mratibu 
Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la 
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini , Alvaro Rodriguez kuelekea 
kwenye ukumbi wa mkutano.
Alisema
 mpango wa muda mrefu umelenga ifikapo mwaka 2025 mchango wa kilimo kwa 
pato la taifa utapungua kutoka asilimia 27.8 kufikia 20.7, mchango wa 
viwanda kupanda kutoka 24.4 hadi 30.7 na mchango wa huduma utapanda 
kutoka asilimia 47.8 ya mwaka 2010 hadi 48.6.
“Ni
 matumaini yangu kwamba wastani wa idadi ya watu ikipungua kutokana na 
elimu na huduma safi za afya au ukuaji wa kasi wa pato la taifa kuliko 
ongezeko la watu na hivyo kipato kitaongezeka na umaskini utapungua”
Miaka 10 iliyopita mchango wa kilimo katika pato la taifa umekuwa mkubwa huku vizazi na vifo vikiwa ni vingi.
Mkutano
 huo ambao unajadili mabadiliko ya kiuchumi kwa ajili ya maendeleo ya 
jamii unatokana na ripoti ya mradi wa maendeleo ya jamii (THDR) 
iliyofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Wageni waalikwa wakipitia ripoti mbalimbali zilizoandaliwa na ESRF nje ya ukumbi wa mikutano kabla ya kuwasili kwa mgeni rasmi.
Naye
 Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika
 la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini , Alvaro Rodriguez 
akizungumza kwa niaba ya Umoja wa Mataifa katika mkutano huo amesema 
Umoja wa Mataifa utaendelea kuisaidia Tanzania kutengeneza ustawi kwa 
wananchi wake.
Alisema
 pamoja na kuwapongeza ESRF kwa kuandaa mkutano huo muhimu wa kuipatia 
serikali fikira za namna ya kuboresha hali za wananchi wake.
Alisema
 amefurahishwa kwa ESRF kusaidia kutafuta mustakabali wa maendeleo kwa 
minajili ya kuendeleza wananchi kwani maendeleo ya kweli ni yale 
yanayoboresha maisha ya wananchi.
Aidha
 alivitaja vigezo muhimu vya maendeleo ya jamii katika hali ya uchumi 
unaokua ambavyo ni kuhakikisha kwamba kuna usawa katika ukuaji wa uchumi
 na maisha ya wananchi, kuongeza uwezo wa kuhami maendeleo yaliyofikiwa 
dhidi ya haki zisizotabirika zinazovuruga ustawi,Kuhakikisha maendeleo 
endelevu ya wananchi na nchi na kuendelea kuwasaidia wanaume kwa 
wanawake kushiriki kikamilifu katika mchakato wa maendeleo iwe kiuchumi,
 kijamii na kisiasa na kugawana kwa usawa matunda ya maendeleo.
Mratibu
 wa Programu kutoka ESRF, Yasser Manu (kulia) akibadilishana mawazo na 
baadhi ya wafanyakazi wenzake nje ya ukumbi wa mikutano kabla ya 
kuwasili kwa mgeni rasmi.
Amesema
 Mratibu huyo wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini kwamba 
amefurahishwa na taarifa kwamba mkutano huo utajadili mada mbalimbali na
 kutolea ushauri kwa kuzingatia taarifa ya THDR.
Awali
 akimkaribisha Mwenyekiti wa Bodi ya ESRF Philemon Luhanjo, kumkaribisha
 rais Jakaya Kikwete Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF Dk Hoseana Lunogelo 
alisema wakati taasisi hiyo inaadhimisha miaka 20 ya uwepo wake, katika 
mkutano wake wa 3 wa kitaifa wanatarajia wanazuoni kuchambua mada 
mbalimbali na kuandika kitu kitakachosaidia serikali katika kuhakikisha 
maendeleo ya kiuchumi yanakwenda sanjari na ustawi wa jamii kwa maana ya
 kuondokana na umaskini katika ngazi ya mtu mmoja mmoja.
Mada zinazochambuliwa zinatoka kwa wataalamu waliobobea kutoka Tanzania,Ethiopia, Uingereza, Norway na India.
Mkurugenzi
 Mtendaji wa ESRF, Dk. Hoseana Lunogelo akibadilishana mawazo na Balozi 
wa Japan nchini Tanzania,Mh. Masaki Okada wakati wakimsubiri mgeni rasmi
 kuwasili ukumbini hapo.
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete 
akilakiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya ESRF, Philemon Luhanjo mara baada ya 
kuwasili kwenye hoteli ya Hyatt Regency, Kilimanjaro kufungua mkutano 
mkubwa wa tatu wa Taasisi Huru ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF) 
unaozungumzia ukuaji wa uchumi kwa kutumia fursa zilizopo na maendeleo 
yanayogusa jamii.
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete 
akisalimiana na Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na 
mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, 
Alvaro Rodriguez.
Mkurugenzi
 Mtendaji wa ESRF, Dk. Hoseana Lunogelo (kushoto) akiongozana na Rais wa
 Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) 
pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya ESRF, Philemon Luhanjo (katikati) 
kuelekea ukumbi wa mikutano.
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete 
akiwasili ukumbini kufungua mkutano mkubwa wa tatu wa Taasisi Huru ya 
Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF) unaozungumzia ukuaji wa uchumi kwa 
kutumia fursa zilizopo na maendeleo yanayogusa jamii. Katikati ni 
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika 
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez.
Meza
 kuu, Katikati ni mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 
Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya fedha, 
Prof. Adolf Mkenda, Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na 
mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, 
Alvaro Rodriguez ( wapili kulia), Mwenyekiti wa Bodi ya ESRF, Philemon 
Luhanjo (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dk. Hoseana Lunogelo 
(wa pili kushoto).
Mkurugenzi
 Mtendaji wa ESRF, Dk. Hoseana Lunogelo akisoma taarifa ya taasisi yake 
mbele ya mgeni rasmi wakati wa mkutano mkubwa wa tatu wa ESRF 
unaozungumzia ukuaji wa uchumi kwa kutumia fursa zilizopo na maendeleo 
yanayogusa jamii sambamba na kutimiza miaka 20 ya tasisi hiyo tangu 
kuanzishwa kwake uliofanyika jana jijini Dar katika hoteli ya Hyatt 
Regency, Kilimanjaro.
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akitoa 
mkono wa pongezi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dk. Hoseana Lunogelo 
mara baada ya kusikiliza taarifa ya maendeleo ya ESRF.
Mwenyekiti
 wa Bodi ya ESRF Philemon Luhanjo, akizungumza neno fupi kabla ya 
kumrabisha mgeni rasmi Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete Rais wa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania kufungua rasmi mkutano huo.
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete 
akifungua rasmi mkutano mkubwa wa tatu wa ESRF unaozungumzia ukuaji wa 
uchumi kwa kutumia fursa zilizopo na maendeleo yanayogusa jamii 
uliofanyika jana jijini Dar katika hoteli ya Hyatt Regency, Kilimanjaro.
Mkurugenzi
 wa Programu wa ESRF ambaye pia ni Mratibu wa Mradi wa taarifa ya 
maendeleo ya watu nchini Tanzania (THDR), Dr. Tausi Kida akifuatilia kwa
 makini hotuba ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakati wa mkutano huo.
Mjumbe wa Bodi ya wadhamini ESRF, Prof. Sylvia Temu akitoa neno la shukrani kwa mgeni rasmi.
Mratibu
 Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la 
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez 
akizungumza kwa niaba ya Umoja wa Mataifa wakati wa mkutano huo. Kulia 
ni Gelase Mutahaba kutoka Chuo kikuu cha Dar es Salaam, Kushoto ni Prof.
 Bertil Tungodden kutoka nchini Norway na Mjumbe wa Bodi ya wadhamini 
ESRF, Prof. Sylvia Temu (wa pili kushoto).
Pichani
 juu na chini ni Baadhi ya wawakilishi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa 
nchini, mabalozi, taasisi mbalimbali za serikali waliohudhuria mkutano 
huo uliofanyika kwenye hoteli ya Hyatt Regency, Kilimanjaro jijini Dar.
Kwa picha zaidi MOblog.....(MC)























No comments:
Post a Comment