MBUNGE KESSY ASIPIGWE, AJIBIWE HOJA ZAKE

Mbunge wa Nkasi (CCM),  Ally Kessy akisisitiza jambo.
Mbunge wa
 Nkasi (CCM),  Ally Kessy wiki iliyopita  alilazimika kusindikizwa na 
askari wa Bunge la Jamhuri kuondoka katika viwanja vya eneo hilo 
kumnusuru na hasira za wajumbe kutoka Zanzibar waliokerwa na mchango 
wake kuhusu masuala ya Muungano.
Kessy 
alisimama bungeni hapo kutoa mchango wake kuhusu Katiba ya Jamhuri 
akijikita zaidi katika suala la muundo wa Muungano na kusema kwamba 
Zanzibar inabebwa na Tanganyika.
Nimnukuu,
 alisema: “Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanganyika inabeba mzigo mkubwa ambao 
haubebeki, hapa tunahudumia wabunge 83 kutoka Zanzibar ambao wanatibiwa 
wao na wake zao na watoto kwa gharama za Tanganyika wakati hawachangii.”
Aliongeza
 kuwa haiwezekani kwa Tanganyika kubeba mzigo mkubwa kama huo wakati 
katika Jimbo lake la Nkasi wananchi wanalia na shida ya maji.Alisema 
katika kamati yao Namba Moja, Gavana wa Benki Kuu, Profesa Benno Ndulu 
alitoa semina iliyoonyesha kuwa Zanzibar haichangii chochote kwenye 
Serikali ya Muungano na kuwa hata mishahara wakati mwingine wanategemea 
Tanganyika.
Kessy 
alisema wananchi wakilijua jambo hilo, wataikataa katiba inayopendekezwa
 na kuitupilia mbali kwa kuwa inatoa upendeleo kwa Wazanzibari na 
kuikandamiza Tanganyika.GPL (P.T)
“Mimi 
naweza kuwa na wanawake sita, nikazaa nao lakini kila mtoto anaendelea 
kutunzwa na baba yangu, jambo kama hili halivumiliki hata kidogo japo 
najua kuwa ukweli unawauma,” alisema huku baadhi ya wajumbe wakipaza 
sauti wengine kumpinga na wengine kuomba mwongozo wa mwenyekiti.
Lakini 
ninachotaka kusema hapa ni kwamba wananchi wengi wa Tanganyika 
niliozungumza nao katika utafiti wangu usio rasmi wanaungana na mbunge 
huyo.
Hapa Dar 
es Salaam baadhi ya wakazi wanasema iweje Zanzibar yenye watu milioni 
moja na ushee wawe na wabunge 83 wakati jiji lao lina wakazi zaidi ya 
milioni nne na lina wabunge wasiozidi kumi?
Alipinga 
suala la Rais wa Zanzibar kuwa makamu wa rais wa Muungano kwa maelezo 
kuwa katika mfumo wa vyama vingi jambo kama hilo haliwezekani na kuhoji 
itakuwaje awe makamu wa kwanza wa rais wakati hajachaguliwa na wananchi 
wa Tanzania Bara?
Baada ya 
kauli hiyo, kelele za wajumbe kutoka Zanzibar ziliongezeka baadhi 
wakisimama na kuwasha vipaza sauti kumshambulia Kessy hivi: “Chizi huyo,
 chizi huyo, hafai kwanza ni Mwarabu,” zilisikika sauti huku nyingine 
zikimtaka aombe radhi.
Ukweli ni
 kwamba alichokizungumza Kessy ndizo kero za muungano kwa upande wa 
Tanganyika. Kati ya watu 50  niliowauliza jijini Dar kuhusiana na kauli 
hizo, ni wawili tu waliopingana naye, hivyo ni dhahiri kwamba kauli yake
 inapaswa kutazamwa.
Baba wa 
Taifa, Mwalimu Julius Nyerere aliwahi kusema kwamba wachache wakitokea 
na kutoa wazo ambalo baadaye linaweza kuleta vurugu, ni bora 
likakubaliwa kama halina madhara. Hivyo hayo ya Kessy yatazamwe na 
yasipelekwe kisiasa.
Sikuona 
sababu za wajumbe kutoka Zanzibar kumshambulia Kessy wakati aliyesema 
hayo ni Gavana wa Benki Kuu, Bwana Ndulu yeye alikuwa akirudia na ndiyo 
maana akasema hayupo tayari kuomba radhi.
Alidai 
Ndulu alikuja katika kamati na akasema kwamba tangu kifo cha Abeid 
Karume (rais wa kwanza wa Zanzibar), Zanzibar hawajawahi kuchangia 
muungano, hili lilikuwa ndilo la msingi la kulijadili kama ni kweli au 
ni uzushi na siyo kuzomea na kutaka kumpiga mtoa hoja.
No comments:
Post a Comment