RAIS KIKWETE HAWEZI KUAHIRISHA BUNGE
Mjumbe
 wa Bunge Maalum la Katiba, ambaye ni  Mwenyekiti wa Kituo cha 
Demokrasia Tanzania(TCD)Mhe. John Cheyo amesema kwamba mchakato mzima wa
 Katiba utamalizwa kwa kura ya maoni ya wananchi, hivyo Rais wa Jamhuri 
ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Jakaya  Kikwete haiwezi kutamka leo 
kuliahirisha Bunge Maalum la Katiba kwa kuwa liko Kisheria.
Aidha
 Mhe. Cheyo alisema kilichoahirishwa ni mchakato wa kura ya maoni ya 
wananchi na si Bunge hilo kwa kuwa walikubaliana   katika kikao cha 
mashauriano, baina Rais Kikwete na  Viongozi  Wakuu wa Vyama vya Siasa 
vyenye wabunge vinavyounda TCD kuwa bunge hilo liendelee. 
Kauli
 hiyo imetolewa leo Bunge Mjini Dodoma na Mhe. Cheyo wakati wa mjadala 
wa kujadili sura zilizobakia za Rasimu ya Katiba Mpya, ambapo alisema 
hayo ndiyo makubaliano yaliyofikiwa.
 Aidha Mhe. Cheyo alisisitiza Katiba Mpya inayopendekezwa itakayopatikana itadumu kwa njia ya maridhiano.
“
 Bunge hili linaendeshwa kwa mujibu wa sheria , Tangazo la  Serikali 
(Government Notice) Na 254 hili ndilo uhai wa Bunge hili hadi Oktoba 4, 
mwaka 2014, na wote tukakubaliana haiwezekani   Mhe. Rais akasema   leo 
Bunge likasitishwa.
“
 Vitu viwili vikukutana  kwa nia ya maridhiano, vitu vingine vinaweza 
kuwekwa pembeni sawa na sasa na baadae vinaweza vinashughulikiwa kwa 
wakati huo,” alisema Mhe. Cheyo.
Mhe.
 Cheyo alisema anamwomba  Rais Kikwete atoe ruhusa ya kuwepo kwa kipindi
 maalum  cha kitakachorushwa na televisheni (video) ili kila mtu 
aonekana alichokisema, huku akionesha kusikitishwa na upotoshwaji wa 
makubaliano hayo, uliofanywa na baadhi ya wanasiasa.
 “
 Mojawapo  ambayo tuliyokubaliana  Bunge hili lipate Katiba ambayo 
inapendekezwa na wananchi pia kwa hali tulinayo haiwezekani  mchakato 
mzima ukamalizika, mchakato utamalizika kwa kura ya maoni  ya wananchi. 
Kama tukifika  huko itabidi tuhairishe uchaguzi wa mwaka 
2015.   Niliyoyasema  ndiyo makubaliano tuliyokubaliana,” alisisitiza.
Mhe. Cheyo alisema Rais Kikwete alikubali kukaa chini pamoja na TCD na hao wanaojiita Ukawa.
 Alisema  Rais
 Kikwete alifanya mazungumzo na  viongozi wa Vyama vya Siasa vyenye 
wabunge vinavyounda TCD  mara  kwa mara ya kwanza, Agosti 31, mwaka 2014
 kwa saa nne na mara ya pili, Septemba 8, mwaka 2014 kwa  saa mbili. 
Kikao
 hicho cha mashauriano kilihusisha  kamati ya makatibu wakuu,  kamati ya
 wenyeviti wa vyama  vya CCM, CHADEMA,CUF na NCCR-  Mageuzi.
(Awadh Ibrahim)
No comments:
Post a Comment