TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, January 8, 2014

MORSI ACHELEWA KUWASILI MAHAKAMANI MISRI

Taarifa kutoka Misri zinasema kiongozi aliyepinduliwa nchini humo, Mohammed Morsi, amechelewa kuwasili mahakamani leo mjni Cairo.
Inasemekana kuwa hali mbaya ya anga imeizuia helikopta iliyotarajiwa kumsafirisha hadi katika mji mkuu huo anakokabiliwa pamoja na maafisa wengine wa utawala wake na tuhuma za kuchochea mauaji ya waandamanji mnamo mwaka 2012 alipokuwa madarakani.
Awali vikosi vya usalama viliimarisha ulinzi katika mji mkuu wa Misri Cairo ,Morsi akitarajiwa kuwasili mahakamani.
Yeye na maafisa kadhaa wa serikali yake wanashutumiwa kuchochea ghasia na kuwauwa waandamanaji mwaka 2012 wakati wa utawala wake. Mashitaka hayo ni pamoja na kushirikiana na wanamgambo wa kigeni kuvunja gereza.
Aling'olewa madarakani kwa mapinduzi mwezi julai mwaka jana na kufungwa . Alipofika mahakamani Mwezi Novemba mwaka jana bwana Morsi alisema kuwa bado yeye ni Rais na alifungwa kinyume na matakwa yake.(P.T)

No comments:

Post a Comment