TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Sunday, January 5, 2014

HAYA NDIYO MAAMUZI YA KAMATI KUU YA CHADEMA 

Katibu Mkuu anaanza kwa kuomba radhi kwa kuchelewa kuanza press akiungana na John Mnyika pia Katibu Mkuu anasema kuwa atasoma neno kwa neno kutokana na umuhimu wa hoja yenyewe! Ameanza kusoma na kusema kamati kuu ilikuwa ni ya dharura iliyokuwa na lengo la kuwajadili Wanachama watatu Dr. Kitila Mkumbo, Zitto Kabwe na Samsoni Mwigamba.
Dr Slaa anaonyesha kabrasha lenye nyaraka mbalimbali ikiwemo mkakati wa mabadiliko 2013, mashtka ya watuhumiwa na nyaraka nyingine muhimu. Sasa Dr. Slaa anasoma mashtaka yote 11 ya Watuhumiwa kama walivyokabidhiwa kwa maandishi
Katibu Mkuu anasema Watuhumiwa wawili yaani Dr. Kitila Mkumbo na Samsoni Mwigamba waliitikia wito wa Kamati Kuu lakini aliyehojiwa na Kamati Kuu ni Dr. Kitila Mkumbo pekee ambaye katika utetezi wao walikana kuvunja katiba ya Chama na Kanuni zake.
Katibu Mkuu anasema Dr Kitila Mkumbo alikiri kumfahamu M2 na anamjua fika lakini hawezi kumtaja mpaka awasiliane nae kwanza. Pia Dr Kitila Mkumbo alisema yeye na Mwandishi wa waraka ule walimpa briefing Mh. Zitto Kabwe kwa hiyo alikuwa anaufahamu waraka huo.(P.T)
Dr. Kitila Mkumbo alikataa kuzungumzia vifungu vya katiba walivyodai vimevunjwa kwa madai kuwa tayari wana malalamiko kwa msajili tayari. Aidha Dr. Kitila Mkumbo alishindwa kuithibitishia Kamati Kuu kwa ushahidi kuhusu madai ya taarifa ya fedha ambazo yeye na Zitto walishiriki, pia alishindwa kuonyesha ushiriki wa M/Kiti katika manunuzi ya vifaa mbalimbali vya Chamazikiwemo pikipiki za Chama.
H...ivyo Kamati Kuu imeamua kuwavua Uanachama ndugu Samsoni Mwigamba na Dr. Kitila Mkumbo kuanzia tarehe ya jana baada ya maamuzi ya kikao cha Kamati Kuu. Maamuzi hayo ni baada ya kunasa mawasiliano mbalimbali ya Zitto Kabwe na washirika wake akiwemo anayejulikana kwa jina la Chadema Mpya.
Dr. Slaa anasema malengo ya waraka wa mabadiliko hayakuwa ya kisiasa tu bali yalikuwa na lengo la kuimaliza chadema na kuwabomoa Viongozi wa Chama.
Mwisho
Chama kinawatangazia Wanachama wote na wapenzi wote kutokushiriki mikutano ama shughuli zozote za kisiasa zitakazoandaliwa na Zitto Kabwe na Washirika wake kwa jina la Chama.

No comments:

Post a Comment