TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, January 30, 2014

BANDARI DAR KUPAKUA MIZIGO TANI MILIONI 18 

BBBBBBB_d1c95.jpg 
BANDARI ya Dar es Salaam kwa kupitia mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN), inatarajia kupakua mizigo tani milioni 18 ifikapo mwaka 2015 kutoka tani milioni 13.5 wanayopakua sasa.
Aidha,wanatarajia kuboresha bandari ndogo za kwenye maziwa kuongeza ufanisi wa kutoa mizigo ikiwemo kuongeza ufanisi wa Usafiri wa Reli ambao kwa sasa unatoa bandarini asilimia 1.2 ya mizigo tu.
Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Awadhi Massawe alimweleza hayo Waziri Mkuu wa Finland, Jyrki Katainen alipotembelea bandari hiyo, ikiwa sehemu ya ziara yake ya siku mbili nchini iliyomalizika jana.
Massawe alikuwa akielezea mafanikio na changamoto zinazoikabili bandari hiyo na kubainisha kuwa ifikapo mwaka 2028 wanatarajia kupakua tani milioni 41.5 za mizigo.
Akizungumza bandarini hapo, Katainen alisema amefurahishwa na uamuzi wa Serikali kuipa kipaumbele uboreshaji wa bandari kupitia mpango wa BRN kwani ikiwa na uwezo wa kutoa stahili pia biashara nchini itakuwa imara.
Wakati huo huo, Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyere aliwahakikishia watumiaji wa Bandari ya Dar es Salaam kuwa ni salama katika usafirishaji, uhifadhi na udhibiti wa kemikali mbalimbali hasa zile za salfa.
Alisema tangu mwaka 2003 kumekuwa na sheria ya kudhibiti usafirishaji na uhifadhi wa kemikali nchi nzima. Katika bandari hiyo alisema upo uangalizi maalumu.
CHANZO:HABARILEO

No comments:

Post a Comment