TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, July 18, 2014

Unamkumbuka Rapa aliyejikata sehemu za siri?kaja na hii mpya

johnson
Mwezi April ilisambaa stori juu ya mwanamuziki wa Hip Hop Andre Johnson kujikata sehemu zake za siri ambapo stori hiyo iliripotiwa na vyombo kadhaa duniani lakini mbali na kujikata sehemu hizo alijirusha kutoka juu ya jumba moja mjini Los Angeles.
Ukubwa wa stori hii umefanya wadau mbalimbali wa vyombo vya habari kutaka kufahamu sababu za yeye kuamua kufanya vitendo hivyo ambavyo pengine vinaashiria hata kuyagharimu maisha yake.
Johnson ametoa sababu zake na kubwa zaidi akisema kuwa yeye ana akili timamu hana matatizo ya akili ingawa aliwahi kutumia dawa za kulevya lakini alikuwa anajifahamu mahojiano hayo ameyafanya kupitia kituo cha televisheni cha E! kilichopo Marekani.
Sababu nyingine aliyoisema kwenye mahojiano hayo amesema kuwa yeye sio Mwandamu>>’Nilikata sehemu yangu ya siri kwa sababu hiyo ndiyo ilikuwa chanzo cha matatizo yangu’
‘Suluhu yangu kwa matatizo yangu ni kwamba nimeelewa kuwa kitendo cha ngono ni cha mwanadamu, mimi sio mwanadamu mini ni mungu vitendo vya ngono viliniingiza katika matatizo mengi.siko hapa duniani kama mwanadamu bali mungu ”
Madaktari walishindwa kuunganisha sehemu hizo za siri za Johnson na kwa sasa anaishi bila sehemu hizo za siri na kusema kuwa anafurahi yuko hai,hilo ndilo jambo muhimu zaidi kwake, hata bila ya uume wake.

No comments:

Post a Comment