TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Saturday, July 5, 2014

BRAZIL WAIPIGA COLOMBIA 2-1 NA KUTINGA ROBO FAINALI 

article-2681056-1F65BFA200000578-434_634x422
Beki wa Brazil,  David Luiz aliachia shuti kali la mpira wa adhabu na kufunga bao la pili na la ushindi.ULIKUWA usiku mkubwa kwa Wabrazil wakishuhudia vijana wao wa Samba wakicheza mechi ngumu ya robo fainali ya kombe la dunia dhidi ya timu ya Colombia.Haikuwa rahisi kuwazuia Wabrazil waliokuwa na morali ya kushinda mechi ya leo na kuungana na Ujerumani iliyofuzu nusu fainali kwa kuifunga Ufaransa bao 1-0 katika mchezo wa kwanza.Usiku huu kumekuwepo na maendeleo, shukurani kwa bao la mapema la Thiago Silva (dakika ya 7) lililowachanganya Colombia.Ulikuwa mchezo mkali na wenye kasi kwa dakika zote 90, lakini bao la pili lililofungwa na David Luiz kwa shuti kali la mpira wa adhabu katika dakika ya 68 liliwaamusha Wabrazil kwa mara nyingine tena.Alikuwa kijana mkali, James Rodriguez aliyeifungia Colombia bao la kufutia machozi kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 80, lakini yote kwa yote, Wacolombia ndio `bai bai` tena.
Pick that one out! Luiz celebrates after hitting an incredible free-kick past Colombia goalkeeper David Ospina
Luiz akishangilia baada ya kufunga goli kwa shuti la mpira wa adhabu lililomuacha kipa wa Colombia, David Ospina akiambulia manyoya tu.
Special strike: David Luiz points to the goal following his strike as Paulinho looks on and smiles
 David Luiz akimshukuru Mungu wake baada ya kufunga, huku Paulinho akimtazama kwa tabasamu. (P.T)
Opener: Thiago Silva bundles the ball in at the back post to give Brazil the lead against Colombia in Fortaleza
 Bao la ufunguzi: Thiago Silva akifunga bao la kuongoza la mapema dhidi ya Colombia.

Proud moment: Brazil defenderThiago Silva beat his chest after giving his country the lead after seven minutes
 Beki wa Brazil, Thiago Silva akishangilia baada ya kufunga.
Kikosi cha Brazil: Julio Cesar, Maicon, Thiago Silva, Luiz, Marcelo, Fernandinho, Paulinho, Oscar, Neymar, Hulk, Fred. 
Wachezaji wa akiba: Jefferson, Dani Alves, Dante, Maxwell, Henrique, Ramires, Hernanes, Willian, Bernard, Jo, Victor.
Wafungaji: Thiago Silva, 7, David Luiz, 68.
Kikosi cha Colombia: Ospina, Zuniga, Zapata, Yepes, Armero, Guarin, Sanchez Moreno, Cuadrado, Rodriguez, Ibarbo, Gutierrez. 
Wachezaji wa akiba: Vargas, Arias, Carbonero, Aguilar, Mejia, Balanta, Bacca, Ramos, Quintero, Martinez, Valdes, Mondragon.
Mfungaji: Rodriguez (pen), 80.
Mwamuzi: Carlos Velasco Carballo (Spain)

No comments:

Post a Comment