TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, July 17, 2014

TETESI ZA SOKA ULAYA 

Chelsea wapo tayari kumuuza John Obi Mikel, 27, wakati wanapanga kumnyatia kiungo wa Real Madird Sami Khedira, 27 ambaye pia anatakiwa na Arsenal (Daily Express), Arsenal wanatarajia kuthibitisha siku la Alhamisi usajili wa kiungo wa Newcastle Mathieu Debuchy, 28, kwa pauni milioni 10 (London Evening Standard).
Tottenham watampa beki Jan Vertonghen, 27, mkataba mpya wa miaka mitano, pamoja na kuongeza mshahara hadi pauni 45,000 kwa wiki (Daily Mail), boss mpya wa Manchester United Louis van Gaal anataka kuwaondoa takriban wachezaji kumi wakiwemo Ashley Young, Patrice Evra, Fellaini, Nick Powell, Anderson, Javier Hernandez, Wilfried Zaha, Nani, Tom Cleverly, Chris Smalling na Bebe (Daily Star na Daily Mirror).(P.T)
Mark Hughes wa Stoke City yuko karibu kumchukua winga wa Liverpool Oussama Assaidi, 25 kwa uhamisho wa takriban pauni milioni 7 (Daily Telegraph), meneja wa QPR Harry Redknapp anapanga kumchukua beki wa kati wa Aston Villa Ron Vlaar kwa pauni milioni 4 (Birmingham Mail), Liverpool watapambana na Tottenham kumwania beki wa kushoto wa Swansea Ben Davies (Daily Star).
Toni Kroos anajiandaa kuhamia Real Madrid kwa mkataba wa euro milioni 30 akitokea Bayern Munich (Bild). Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Share tetesi hizi na wapenda soka wote. 
Kutoka kwa Salim Kikeke

No comments:

Post a Comment