TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Saturday, July 5, 2014

UJERUMANI NA CHINA :UHUSIANO MAHSUSI?

Angela Merkel na Rais wa China Xi Jinping
Kansela Angela Merkel na Rais wa China Xi Jinping
China na Ujerumani zinatarajia kutiliana saini mikataba kadhaa wakati wa ziara ya Kansela wa Ujerumani Angela Merkel inayoanza Jumapili nchini China.
Ni katika mwezi wa Machi tu ambapo Rais wa China Xi Jinping aliafanya ziara nchini Ujerumani.
Na mapema mwaka huu Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier alikuwapo China kwa ajili ya ziara.Na katika msimu wa mapukutiko baraza lote la mawaziri la China litakuwapo nchini Ujerumani kwa ajili ya mashauriano ya kiserikali. Licha ya hatua hizo zote zaira ya Kansela wa Ujerumani inafuatia.
Hakuna kiongozi mwengine yeyote wa Ulaya anaekutana na viongozi wa China mara kwa mara kuliko Kansela wa Ujerumani Angela Merkel. Uhusiano baina ya Ujerumani na China unasonga mbele kwa nguvu.Na ili kuidumisha kasi Kansela Merkel sasa anaitembelea China.(P.T)
Katika ziara hiyo mikataba kadhaa itatiwa saini baina ya Ujerumani na China juu ya mambo ya tekinolojia, elimu na utamaduni. Kansela Merkel ataianzia ziara yake ya siku tatu katika jimbo la Sichuan la kusini magharibi mwa China.Jimbo hilo lina idadi ya wakaazi sawa na Ujerumani.
Kwa muda wa karibu miaka 10 Ujerumani imekuwa inakimu ubalozi katika mji mkuu wa jimbo hilo, Chengdu. Sababu ni kwamba mji huo ni daraja la kuingilia katika jimbo la Sichuan kwa makampuni ya Ujerumani.Jimbo hilo la magharibi linahesabika kuwa na maendeleo hafifu. Makampuni karibu 160 ya Ujerumani yanawakilishwa katika jimbo hilo.Kansela Merkel ataitembelea kampuni ya magari ya VW.
Jumapili jioni Kansela Merkel ataenda Beijing ambako atakutana na Waziri Mkuu wa China Li Keqiang. Hapo Jumatatu kiongozi huyo wa Ujerumani atakutana na Rais Xi -Jinping ambae pia ni Mwenyekiti wa chama cha kikomunisti kinachotawala China.
Profesa wa masuala ya Ujerumani kwenye chuo kikuu cha lugha za kigeni cha mjini Beijing Liu Liqun anataraji kwamba viongozi hao watayazungumzia masuala ya kiuchumi.
Kitovu cha mazugumzo ni masuala ya kiuchumi
Kwa mara ya kwanza kamati mpya ya mashauriano ya masuala ya kiuchumi itakutana mjini Beijing ambapo Kansela Merkel na Waziri Mkuu wa China Li Keqiang watakuwapo.Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa taasisi ya mitaala ya China Sebastian Heilmann, kamati hiyo itayafafanua masuala ya kiuchumi yanayozihusu nchi mbili hizo na kutoa mapendekezo kwa viongozi. Serikali za Ujerumani na China zitayashughulikia mapendekezo hayo kwa kuchukua hatua thabiti.
Hati miliki
Katika mahojiano na DW, mtaalamu wa China wa masuala ya Ujerumani Liu Liqun amekiri kwamba yapo matatizo katika upande wa China kuhusiana na ulinzi wa hati miliki.Amesema kwamba katika miaka ya hivi karibuni mengi yameboreshwa lakini hatua zilizochukuliwa hazijatosha. Amesema matatizo yanaweza kutokea katika utekelezaji wa mradi wa uhaulishaji unaopewa kipaumbele pia na China.
Mwaka ujao unaazimiwa kuwa wa kuutekeza mradi wa ushirikiano katika uhaulishaji baina ya Ujerumani na China.
Haki za binadamu
Ilifahamika hata kabla ya Merkel kuanza ziara kuwa suala la haki za binadamu litazungumziwa .Katika suala hilo bado pana mapungufu mengi katika upande wa China. Hata hivyo masuala hayo yatajadiliwa kwenye vikao vya faragha kwa uthabiti na hata kwa hoja za mabishano ,mkasa kwa mkasa utajadiliwa.
Kwa mujibu wa taarifa Kansela Merkel atampigania mwanaharakati Ai Weiwei ili apewe kibali cha kuondoka nchini China. Kwa muda wa miezi kadhaa sasa mwanaharakati huyo ambae pia ni msanii amekuwa anatumai kuondoka China na kuenda Ujerumani.Msanii huyo bado ameshikiliwa mjini Beijing na idara husika. Kwa sasa maonyesho ya kazi zake za kisanii ambayo ni makubwa kabisa kuwahi kufanyika yanaendelea mjini Berlin.
Mwandishi von Hein,Matthias
Tafsiri:Mtullya Abdu
Mhariri:Ssessanga Iddi
Chanzo:http://www.dw.de/

No comments:

Post a Comment